Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema katika miaka michache, Dkt John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania ameonesha kuwa Waafrika wana uwezo wa kujitoa katika utegemezi wa watu na vitu vya nje
Amesema, "Kwa muda mfupi tumeona kazi ya barabara, ujenzi wa Uwanja wa Ndege na mambo mengine mengi ambayo yatakuwa na manufaa kwa Watanzania na wana Afrika Mashariki"
Rais Kenyatta amemuelezea Hayati Dkt. Magufuli kama Rafiki wa karibu ambaye walikuwa wanaongea mara kwa mara. Amesema kifo chake ni pigo kwasababu alikuwa mtu wa heshima
Ameongeza, "Nawahakikishia tutaendelea kufanya kazi pamoja, tutaendelea kushirikiana na kuhakikisha tunaleta pamoja Jumuiya ya Afrika Mashariki"