Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Felix Tshisekedi amwagiwa pongezi za ushindi

Rais Felix Tshisekedi Amwagiwa Pongezi Za Ushindi Rais Felix Tshisekedi amwagiwa pongezi za ushindi

Mon, 1 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Jamii ya kimataifa inaendelea kutuma ujumbe wa pongezi kwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia ushindi wa Rais Felix Tshisekedi kwenye uchaguzi mkuu wa Desemba 20, 2023.

Kiongozi wa Umoja wa Afrika na Rais wa Comoros Azali Assoumani alikuwa miongoni mwa viongozi wa kwanza kumpongeza rais Tshisekedi kwa ushindi wake wa asilimia 73.34 ya kura zilizopigwa katika uchaguzi mkuu.

Kutoka jumuiya ya Afrika Mashariki, Rais wa Burundi , Evariste Ndayashimiye alituma ujumbe wake wa heri njema kupitia mtandao wa kijamii wa X na kuomba amani kudumu baada ya ushindi huo kutangazwa.

Katika ujumbe wake, kiongozi huyo wa zamani wa jumuiya ya EAC aliwataka wote wenye kupinga matokeo yaliyotangazwa, ‘kuwasilisha kesi mbele ya mahakama kupitisa njia zinazofuata muongozo wa sheria.’

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga naye, amemtakia Rais Tshisekedi kila la kheir anapoanza muhula wake wa pili madarakani.

‘Ninamuombea uongozi wake ulete mabadiliko mema na mafanikio katika taifa hilo. Nawatakia raia wa DRC kila la kheri katika juhudi zao kujiinua upya , kuidhibiti na kuendeleza taifa lao,’ alisema Odinga.

Tshisekedi alishinda uchaguzi huo ulioandaliwa Desemba 20, 2023 kwa kura zaidi ya milioni 13 ambazo ni asilimia 73 ya jumla ya kura zilizopigwa katika uchaguzi huo. Mpinzani wake wa karibu alikuwa Moisee Katumbi aliyepata kura milioni 3 ambazo ni asilimia 18 ya kura zilizopigwa huku Martin Fayulu aliibuka nambari tatu kwa kura laki tisa ambazo ni asilimia tano ya kura zote zilizopigwa.

Tshishekedi alikuwa anakabiliana na wagombea 19, akiwemo mmoja wa kike, Ifoku Marie-Josee Mputa Mpunga ambaye amekubali kushindwa na kumpa kongole mshindani, Rais Tshisekedi.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye kurasa yake ya mtandao wa kijamii wa X, Marie alisema kwamba, ‘ushindi wake Tshisekedi unaonyesha imani ya raia wa DRC katika uongozi wake.’

Katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, ujumbe wa heri njema kutoka Tanzania, umetumwa Kinshasa huku Rais Samia Suluhu Hassan pia akichapisha salamu zake kwenye mtandano wa kijamii wa X.

‘ Nina matumaini kwamba tutaendelea kufanya kazi kwa karibu na kuboresha uhusiano kati ya mataifa yetu mawili,’ alisema Rais Samia.

Kiongozi wa upinzani nchini Ufaransa, Marine Le Pen, mbali na kutuma ujumbe wa heri njema na kumpongeza rais Tshiekedi, alitaja pia, ‘ Ninawatumia raia wa DRC heri njema na duah ya amani. Hasa wanaokabiliwa na vita ambavyo vinasahaulika katika jimbo la Kivu,Ufaransa ni sharti isimame na taifa hilo, alisema Le Penn.

Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa katika ujumbe wake wa kumpongeza Rais Tshisekedi, aliwapongeza raia wa DRC kwa kuwa watulivu na kuonyesha umoja wakati walipo subiri matokeo rasmi kutangazwa.

Aidha, rais huyo amesema kwamba ,’ Ninaomba utulivu hasa ikiwa kunaye kiongozi ambaye atapinga matokeo hay ana kuwataka wote kutumia njia za kisheria kulingana na katiba ya nchi hiyo kuwasilisha malalamishi yao rasmi,’ alisema rais ramaphosa.

Awali, ujumbe uliotumwa kwenye kurasa ya mtandao wa kijamii wa X ya rais mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta, ukimpongeza rais Tshishekedi, ulifutiiliwa mbali na kutajwa kama usio sawa.

Katika ujumbe huo, Rais Kenyatta alimtaka yeyote kuwasilisha malalmiko yake kupitia njia za Mahakama huku akitaka amani idumu katika eneo la mashariki mwa DRC.

Katika ujumbe wake wa mwisho wa mwaka Rais wa Rwanda Paul Kagame aliwaka tu kuwa na hali ya usalama katika taifa jirani na kusema kwamba Rwanda inatizama suala hilo kwa uangalifu.

Chanzo: Bbc