Mon, 22 Mar 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Felix Tshisekedi ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa nchi za Afrika amesema kuwa Dk John Pombe Magufuli alikuwa kiongozi mwenye maono kwenye uchumi wa Afrika.
Rais Tshisekedi ameyasema hayo alipokuwa akitoa salamu za rambirambi leo Dodoma ambapo alisema Magufuli kuwa ameacha alama Afrika na kuna mengi ya kujifunza na kuyafanya ili kumuenzi.
Ameongeza pia Hayati Magufuli aliifanya Afrika iheshimike tena na pia ametimiza ndoto za waasisi wa nchi barani Afrika.
“Pumzika kwa Amani Magufuli, “ alimalizia Rais huyo wa DRC
Chanzo: www.habarileo.co.tz