Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila si mtu wa kuaminika siwezi kuungana naye 2022, Mudavadi asema

0fgjhsbuiieu7076c Raila si mtu wa kuaminika siwezi kuungana naye 2022, Mudavadi asema

Mon, 14 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Hii ni kufuatia kinara wa ODM, Raila Odinga na mwenzake wa Wiper Kalonzo Musyoka kutangaza kuwa watafufua NASA 2022Mudavadi alisema kuwa Raila si mtu wa kuaminika kwa hivyo hawezi kuungana na muungano wa NASA tenaMuungano wa NASA uliporomoka baada ya Raila kufanya mazungumzo kisiri na kutangaza kushirikiana na Rais Uhuru Kenyatta mnamo Machi 2018Habari Nyingne: Magazeti Jumatatu, Juni 14: Ruto Awatumia Mawaziri Kumfichulia Siri za Uhuru

Kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi amepuzilia mbali uwezekano wa kufufua muungano wa National Super Alliance (NASA) katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Hii ni kufuatia kinara wa ODM, Raila Odinga na mwenzake wa Wiper Kalonzo Musyoka kutangaza kuwa wataungana ili kumshinda Naibu Rais William Ruto katika kinyang’anyiro cha urais 2022.

Lakini Mudavadi, akizungumza mjini Mombasa Jumapili, Juni 13, alisema kuwa Raila si mtu wa kuaminika kwa hivyo hawezi kuungana na muungano wa NASA tena.

"Nataka Wakenya wajue kwamba kuna ukosefu mkubwa wa uaminifu katika muungano wa NASA ambao hauwezi kurekebishwa. Sisi tunataka kwenda mbele. Tuliunda NASA lakini ukweli usemwe hakuna uaminifu."

"Kwa hivyo kama unataka kuturudisha huko na hautaki kukubali kuwa hakuna uaminifu unatarajia tukuamini vipi ukisema unataka kuungana nasi. Tuambie watu ukweli," alisema Mudavadi alipohudhuria ibada katika Kanisa la Pentecostal Assemblies of God, Likoni katika kaunti ya Mombasa.

Habari Nyingine: Spika Muturi Ahofia Wazee Watamvua Wadhifa wa Msemaji wa Mlima Kenya

Muungano wa NASA uliporomoka baada ya Raila kufanya mazungumzo kisiri na kutangaza kushirikiana na Rais Uhuru Kenyatta mnamo Machi 2018 bila kuwajulisha wenzake.

Kulingana na Mudavadi usaliti ulijitokeza wazi wakati vyama tanzu vilinyimwa pesa na wanachama wao kung'olewa katika kamati za bunge.

Hii ni baada ya Seneta wa Kakamega Cleophas Malala kufurushwa kwenye wadhifa wa wachache Seneti.

Huku matamashi yake yakionekana kumshambulia Raila, Mudavadi alisema hana haja ya kuungwa mkono na mtu mwenye ushawishi kufaulu kisiasa.

Muungano wa NASA unajumuisha Kalonzo Musyoka(Wiper), kiongozi wa Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi, kinara wa Ford Kenya Moses Wetang’ula na kiongozi wa ODM Raila Odinga.

Muungano huo ulibuniwa wakati wa uchaguzi mkuu wa 2017 ambapo Raila alipeperusha bendera ya NASA naye Kalonzo akiwa mgombea mwenza.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke