Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila kushiriki uteuzi wa ODM kubaini iwapo atapeperusha bendera ya urais

0fgjhs5s2lurl6b1j Raila kushiriki uteuzi wa ODM kubaini iwapo atapeperusha bendera ya urais

Fri, 16 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga hajatangaza wazi iwapo atawania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa 2022Chama chake kimesema lazima ashiriki uteuzi wa chama iwapo angependa kupeperusha bendera ya urais ya chama hichoSifuna alikanusha madai kwamba baadhi ya wagombea walikuwa tayari wamepokezwa vyeti vya kuwania viti mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa 2022Chama cha ODM kimewahakikishia wafuasi kwamba kila mgombea wa urais atashiriki uteuzi wa chama hata akiwemo kinara wa chama hicho Raila Odinga.

Akizungumza Alhamisi, Julai 15, Katibu Mkuu wa chama hicho Edwin Sifuna amesema kwamba uteuzi wa chama utafanya kwa njia ya haki na huru.

Sifuna alikanusha madai kwamba baadhi ya wagombea walikuwa tayari wamepokezwa vyeti vya kuwania viti mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa 2022.



Read also

Mwakilishi wa Wanawake Laikipia Cate Waruguru Adokeza Kukihama Chama cha Jubilee

" Hakuna yeyote amepewa cheti cha kuwania kiti chochote, hata kiongozi wa chama Raila Odinga pia hajapewa, yeye pia atashiriki uteuzi wa chama na wagombea wengine akiwemo mfanyabiashara Jimmy Wangigi ambaye ameonyesha azma ya kuwania urais," Sifuna aliambia Jalang'o kwenye mahojiano.

Sifuna alisema ingawa Raila amedokeza kuwania Urais lakini hajatangaza rasmi na pia hajatuma ombi la kuwania kiti hicho kwa bodi ya uchaguzi ya chama.

"Raila hajatangaza kwamba atawania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa 2022, hata hatatuma ombi lake kwa bodi ya chama na kutaka apewe tiketi ya kupeperusha bendera ya ODM," Aliongezea Sifuna.

Miongoni mwa wanasiasa wanaotarajiwa kuwania urais kwa tiketi ya chama cha ODM ni mfanyabiasha Jimmy Wanjigi.

Wanjigi ambaye amekuwa akifadhili kampeni za Raila Odinga kwa miaka kadhaa, alishatangaza kwamba atakuwa debeni 2022 kumenyana na Naibu Rais William Ruto na wagombea wengine akiwemo Mukhisa Kituyi.



Read also

Uvumi na Porojo: Wakazi wa Kiambaa Washuhudia Sarakasi Kuamkia Siku ya Kura

Kwa kuwa Wanjigi ni mwanachama dhabiti na mwaminifu wa ODM, ameahidi kutokwenda kinyume na kanuni za chama hicho.

Wanasiasa wengine katika chama cha ODM ambao wametangaza azma ya kuwania kiti hicho ni Gavana wa Mombasa Mombasa Hassan Joho na mwenzake wa kaunti ya Kakamega Wycliffe Oparanya.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke