Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila awahakikishia wafuasi kwamba BBI ingalipo, "Tunaenda Canaan"

731dba0f0d567c65 Raila awahakikishia wafuasi kwamba BBI ingalipo, "Tunaenda Canaan"

Tue, 25 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Raila Odinga amesema ana imani kwamba mpango wa BBI utaendelea na atawaibisha wapinzani wake

- Kulingana na kinara huyo wa chama cha ODM, haya ni majaribio tu kwani yatakuja kuisha

- Wakenya wamemkashifu kwa kukiuka masharti ya covid-19, wakati alifanya mkutano mjini Kisumu, Jumatatu, Mei 24

Kinara wa chama cha ODM Raila Odinnga amewahakikishia wafuasi wake kutoka mkoa wa nyanza kwamba reggea ya BBI itarejea hivi karibu kwa kishindo.

Raila alinukuu Biblia ambapo alijilinganisha na Ayub na Yesu ambao walipitia majaribio na changamoto nyingi lakini mwishowe walishinda.

Akizungumza akiwa mjini Kisumu mtaani Kondole siku ya Jumatatu Mei 24, Raila alisema shetani alimjaribu Yesu akiwa kwenye jangwa, akamjaribu Ayub na magonjwa, kwa hivyo, yeye ana imani kwamba pia atashinda.

" Nawahakikishia kwamba tunaelekea kushinda, kumbukeni hii safari sio rahisi, mambo mengi yanaendelea kutendeka, mkisoma biblia, Ayub alijaribiwa na Mungu, jamaa wake wote waliangamia lakini alisalia imara," Raila alisema.

" Yesu pia alipitia majaribu, shetani aliketi juu ya mlima akiwa jangwani na akaijaribu imani yake. Kwa sasa pia sisi tunapitia majaribio tu, lakini tunakabiliana nayo, wapinzani wetu wanapaswa kujua reggae ya BBI bado itaendelea," Aliongezea Raila.

Hata hivyo, Wakenya wengi walimkashifu Raila kwa kukiuka masharti ya kudhibiti msambao wa virusi vya COVID-19 ikiwemo kukusanya umati mkubwa na kutozingatia umbali wa mita moja.

Baadhi ya Maoni kutoka kwa Wakenya;

Muli Kavolonza Alisema

" Nadhani mikusanyiko mikubwa ilipigwa marufuku, ni wewe unaendeleza msambao wa virusi vya corona mjini Kisumu, hujali hata afya ya wananchi?.

Victor Mukabana naye alisema

" Baada ya miezi miwili, tutaambiwa kwamba virusi hatari kutoka India vinasambaa kwa kasi Kisumu, Mungu okoa Kenya."

" Hii ni ishara ya kuonyesha kufungwa kwa kaunti ya Kisumu ndio tusifanya maadhimisho ya siku kuu ya Madaraka, COVID-19 inaua,"Fred Erick Sags alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke