Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila atapata asilimia 80% ya kura kutoka eneo la Mlima Kenya

57b67a19bb6361ea Raila atapata asilimia 80% ya kura kutoka eneo la Mlima Kenya

Wed, 6 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mbunge mteule wa chama cha Jubilee Maina Kamanda amedai kwamba kinara wa chama cha ODM Raila Odinga atapata zaidi ya asilimia 80% ya kura kutoka eneo la Mlima Kenya katika uchaguzi mkuu ujao.

Maina Kamanda alikuwa miongoni mwa viongozi walioandamana na Raila Odinga katika ziara yake ya siku mbili kaunti ya GarissaAkiwahutubia wakazi, Kamanda alisema kwamba Raila atapata zaidi ya asilimia 80% za kura kutoka eneo la Mlima Kenya.

Kamanda alidai kwamba ni wakati sasa wa Raila kuwa Rais wa 5 baada ya kujaribu mara kadhaa kuwania kiti hicho bila mafanikio.

Akizungumza akiwa kaunti ya Garissa ambapo alikuwa ameandamana na kinara huyo, Kamanda alisema ni wakati wa Raila sasa kuingia Ikulu baada ya kujaribu mara kadhaa bila mafanikio.

Kulingana na Kamanda, Raila kwa sasa amepata umaarufu mkubwa eneo hilo na ana matumaini kwamba mwanasiasa huyo atamrithi Rais Uhuru Kenyatta ambaye tayari amemuidhinisha kuwania urais.

" Kuna wakati ulikuwa pekee yako lakini kwa sasa tuko pamoja, Kamanda akizungumza jua kwamba eneo la Kenya ya kati limezungumza lugha moja. Ningependa kukuhakikishia kwamba unaenda kupata kura zaidi ya asilimia 80% kutoka Mlima Kenya, mara ya kwanza nilikuwa nkisema kwamba tunahitaji tu asilimia 10% lakini kwa sasa tunayo asilimia 80%."Alisema Kamanda.

Kamanda aliongezea kwamba Raila ndiye mgombea bora zaidi wa kumrithi Uhuru akihoji kwamba ataweka msingi bora wa uongozi ikizingatiwa amekuwa katika siasa kwa miaka mingi na ana uzoefu unaohitajika kuliongoza taifa.

" Tunataka Kenya yenye umoja na amani, tunataka viongozi ambao wamepigania nchi yetu kwa muda mrefu, kwa sasa tunaye Rais Joe Biden mwenye umri wa miaka 78 Marekani, Afrika Kusini kulikuwa na Nelson Mandela hapa Kenya tunaye Raila Odinga ambaye tunataka aongoze tu kwa miaka 5." Kamanda Alisema.

Raila alikuwa ziarani kaunti ya Garissa wikendi iliyopita ambapo alikutana na wakazi kujipigia debe huku uchaguzi mkuu wa 2022 ukikaribia.

Waziri huyo wa zamani alikuwa ameandamana na viongozi kadhaa wakiwemo magavana, wabunge na waziri wa hazina ya kitaifa Ukur Yattani.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke