Thu, 13 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiongozi wa Umoja wa Azimio nchini Kenya, Raila Odinga amesema kuwa wanajipanga kwa awamu ya tatu ya maandamano ya kupinga kupanda kwa gharama za maisha nchini humo dhidi ya Serikali.
Odinga ameyasema hayo jana Jumatano, Julai 12, 2023 muda mchache baada ya kusitisha mkutano wake wa hadhara uliopangwa kufanyika katika uwanja wa Kamukunji.
"Tutamlazimisha Ruto (Rais wa Kenya) kuwapa Wakenya mpango mzuri. Hivi karibuni tutawasiliana jinsi awamu ya tatu ya maandamano itakavyokuwa,” amesema.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live