Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila ataka Uhuru achukue mikopo zaidi kugharamia chanjo ya COVID-19

869ec11ee4ab5275 Raila ataka Uhuru achukue mikopo zaidi kugharamia chanjo ya COVID-19

Thu, 22 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila alihofia kuwa taifa hili linakumbana na hatari ya kurudi nyuma kimaendeleo iwapo baadhi ya COVID-19 yataendelea kutekelezwaAlisema Kenya inahitaji kuwachanja yamkini watu milioni 15 ili kurudia hali ya kawaidaWito wa Raila kutaka serikali kuchukua mikopo zaidi inakujia wakati madeni ya taifa yamepita KSh7 trilioni

Kinara wa Upinzani Raila Odinga anaitaka serikali ichukue mikopo zaidi ya kugharamia chanjo ya virusi vya corona ili nchi ifunguliwe.

Akizungumza Jumatano, Julai 21, katika kaunti ya Mombasa, Raila alimtaka Rais Uhuru Kenyatta afungue nchi ili uchumi uanze kustawi baada ya kuathiriwa na janga la COVID-19.

Raila alihofia kuwa taifa hili linakumbana na hatari ya kurudi nyuma kimaendeleo iwapo baadhi ya masharti ya kuzuia maambukizi yataendelea kutekelezwa.

Masharti hayo ni kama vile kafyu na sheria za kuzuia mgusano.

Read also

Magazeti Jumatano, Julai 21: Kilonzo Adai Uhuru Anachezea NASA Shere

“Tunataka zile dawa hata kama zinagharimu pesa ngapi, pesa zitolewe hata kama zinakopwa tukope, hata wabunge wakipandisha kiwango tunachoweza kukopa bora chanjo ije.Pesa pia ipeanwe kwa mama mboga na vijana wetu, ili wananchi wapate pesa mfukoni,” alisema kiongozi huyo wa ODM kama alivyonukuliwa na gazeti la Taifa Leo.

Kigogo huyo wa siasa alikuwa amehudhuria warsha ya kusherehekea Eid-Ul-Adha iliyoandaliwa na Mbunge wa Mvita, Abdulswamad Nassir katika ukumbi wa Bhadalla.

Kulingana waziri mkuu huyo wa zamani, Kenya inahitaji kuwachanja yamkini watu milioni 15 ili kurudia hali ya kawaida, lakini kufikia sasa ni watu milioni 1.6 pekee ambao wamepata chanjo ya COVID-19.

“Wakati huu tuko na shida kwa sababu ya hili janga la corona.Corona imeporomosha uchumi na kuna shida nyingi. Biashara nyingi zimekufa, kuna ukosefu wa kazi na njaa. Namshauri ndugu yangu Uhuru Kenyatta achukue hatua,” aliongezea

Gavana wa Mombasa ambaye pia alihudhuria mkutano huo, alimuunga mkono Raila akisema masharti hayo yanatakiwa kulegezwa kwa sababu yameathiri sekta ya uchukuzi



Read also

Raila Asema Atatumia Mbinu Nyingine Kupitisha BBI Iwapo Itazimwa na Mahakama

Mrundiko wa madeniWito wa Raila kutaka serikali kuchukua mikopo zaidi inakujia wakati madeni ya taifa yamepita KSh7 trilioni.

Hii imepeleka seriklai kuongeza ushuru kwa bidhaa muhimu ili kugharamia madeni hayo.

Mnamo Aprili 2021, serikali ilipewa mkopo wa KSh257 bilioni na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

Mkopo huo ulizua hasira miongni mwa Wakenya wakilalamika kuwa mikopo hiyo, ambayo sasa imegonga KSh8 trilioni ni tisho kwa uhuru wa kitaifa.

Hata hivyo, IMF lilijitetea likisema mkopo uliopeanwa Kenya si wa gharama kubwa, kwani ulizingatia hali ya sasa ya namna taifa hili limelemewa na madeni mengi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke