Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila amjibu Kalonzo: "Nimekwambia uniunge mkono?"

191eea20a0978fe1 Raila amjibu Kalonzo: "Nimekwambia uniunge mkono?"

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila Odinga alisema hajatangaza rasmi iwapo atawania urais au la na kwamba Kalonzo hapaswi kumtangulia kutangaza hiloRaila alisema hajamuomba Kalozo kumuunga mkono kwani sasa anajishuhulisha na masuala ya mchakato wa BBIHaya yanajiri siku moja baada ya kiongozi wa Wiper kusema kwamba atakuwa mpumbavu iwapo atamuunga mkono Raila kwa mara nyingine tenaAliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga amemkabili kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ambaye alisema hatamuunga mkono mara nyingine tena.

Wakati wa mahojiano Jumatano, Juni 16, Kalonzo alisema waziwazi iwapo atamuunga mkono tena Raila ataonekana mmoja wa watu wapumbavu zaidi ulimwenguni.

Kiongozi huyo wa ODM alimjibu Kalonzo wakati wa ziara yake ya pwani Alhamisi, Juni 17, na kusema bado hajatangaza ikiwa atawania urais akiongeza kuwa pia hajaomba kuungwa mkono.

"Je! Nimetangaza kugombea urais? Lakini watu wengine tayari wanasema kuwa hawawezi kuniunga mkono. Je! Nimekuuliza unisaidie? Subiri, hatujafika hapo," alisema wakati akihutubia wakazi wa pwani.

Raila alishikilia kwamba kwa sasa anajihusisha na masuala ya mchakato wa maridhiano (BBI) ambao alisema bado haujafa lakini upo mapumzikoni.

"Mahakama Kuu iliupeleka mchakato wa BBI kwenye mapumziko. Mchakato haukuzimwa," alisema.

Awali TUKO.co.ke iliripoti kuwa Kalonzo alisema hawezi kukubali kumpa Raila usaidizi ifikapo 2022 na ndoa yake na Raila itawezekana akikubali kumuunga mkono.

"Mimi si mwanasiasa dhaifu, na nitakuwa mmoja wa wajinga ulimwenguni iwapo nitakubali kumuunga mkono Raila kwa safari ya tatu bila yeye kurudisha mkono," alisema Kalonzo.

Mtamshi ya Kalonzo yalijiri siku chache baada ya Raila kusema kwamba huenda akashikana tena na Kalozno kuwania urais ifikiapo 2022.

Raila alisema muungano wao utasaidia kuwaangamizwa wanasiasa wenye tamaa ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakila pesa za wananchi.

Vivyo hivyo, Gavana wa Kitui Charity Ngilu pia aliwauliza viongozi hao wawili waungane na kuunda kikosi kitakachomtikisha Naibu Rais William Ruto ambaye tayari ametangaza azma yake ya kuingia Ikulu.

"Ikiwa Kalonzo na Raila watashindwa kuungana kabla ya 2022, basi uwezekano wa Ruto kufanikiwa utakuwa mkubwa," Ngilu alisema wakati akihutubia waombolezaji nyumbani kwa Ndile Mbui Nzau.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke