Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila akosa kuhudhuria maombi ya kitaifa badala yake amtembelea Mukhisa Kitui

F3bc3f21e9d92ea1 Raila akosa kuhudhuria maombi ya kitaifa badala yake amtembelea Mukhisa Kitui

Thu, 27 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga alimtembelea Dkt Mukhisa Kituyi nyumbani kwake jijini Nairobi Alhamisi , Mei 27

- Vigogo hao wamekutana kwa mara ya pili sasa kwa muda usiozidi miezi mitatu, walifanya mkutano wa kwanza Alhamisi, Februari 18

- Kituyi alijiuzulu kama Katibu Mkuu wa kamati ya Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD, ili kushughulikia azma yake ya kuwania urais

Mkutano kati ya kinara wa chama cha ODM Raila Odinga na aliyekuwa Katibu Mkuu wa kamati ya Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD, Mukhisa Kituyi umezua hisia mseto.

Vigogo hao walifanya mkutano huo wakati ambapo viongozi wengi walikuwa wamehudhuria hafla ya maombi ya kitaifa katika majengo ya bunge.

" Nilikuwa na wakati mwema nilipowatembelea Dkt Mukhisa Kituyi na mkewe Ling Nyumbani kwao, tulijadiliana masuala kadha wa kadha. Nilifurahi sana kuona familia hii baada ya muda mrefu," Alisema Raila.

Hata hivyo, hii ilikuwa mara ya pili kwa viongozi hao kukutana, mara ya kwanza ilikuwa kwenye mkahawa mmoja jijini Nairobi siku ya Alhamisi, Februari 18.

" Nimefurahia kukuona Dkt Kituyi baada ya muda mrefu kwa kutokuwa nyumbani," Raila alisema kwenye mkutano wao wa kwanza.

Huenda vigogo hao wakamenyana katika kinyang'anyiro cha urais katika uchaguzi mkuu ujao wa 2022.

Kituyi alijiuzulu kama Katibu Mkuu wa kamati ya Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD, ili kushughulikia azma yake ya kuwania urais, muhula wake ulikuwa ukamilike Septemba 2021.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, Kituyi aliwasili nchini Februari 14 kabla ya kufululiza hadi katika kanisa la Friends Church mtaani Makadara kwa ibada ya shukrani.

Huo ndio ulikuwa wakati wa kwanza wa Mukhisa kutangaza azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi wa 2022.

"Niko tayari kuhudumia taifa hili ikizingatiwa kwamba nina ujuzi wa kimataifa sasa, sio siri tena, nitakuwa kwenye debe katika uchaguzi mkuu wa 2022, hakuna mtu anapaswa kutushauri ni nani tunapashwa kumuunga mkono," Alisema Kituyi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke