Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila ajitambulisha kama Rais awamu ya tano Kenya

2eb0f22f7767ffd9 Raila ajitambulisha kama Rais awamu ya tano Kenya

Sun, 9 Jan 2022 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila alisema rais wa tano atakuwa ni yeye ifikapo mwezi Agosti wakati Wakenya watapiga kuraAlifichua pia kuwa yeye hupenda kumnunulia bae wake maua yaliyong'aa kwa rangi nyekundu kama zawadi ya penzi lakeWadadisi wa kisiasa wanasema uchaguzi wa mwaka huu kuingi Ikulu ni kati ya DP Ruto na Raila

OdingaKinara wa ODM Raila Odinga ameelezea imani yake kuwa mwaka huu atafaulu kuingia Ikulu baada ya uchaguzi wa urais wa Agosti.

Kwenye mahojiano aliyochapisha katika mtandao wake wa Facebook, Raila aliulizwa ni nani atakuwa rais wa tano wa Kenya.

"Ni nani atakuwa rais wa tano wa Kenya," Raila anaulizwa.

"Ana majina tofauti, moja anaitwa Tinga, mara nyingine akaitwa Agwambo na nyingine akaitwa Baba," alisema Raila.

Wafuasi wa Raila hupoenda kumdekeza kwa majina hayo ambapo Tinga lilitokana na alama aliyotumia hapo awali kwenye uchaguzi wa urais.

Aidha kwenye mahoajino hayo, Raila alifungua roho kuhusu mavazi anayoyapenda pamoja na zawadi ambazo humkabidhi Mama Ida.

"Anapenda maua, na rangi yake kuwa anapendelea sana nyekundu," Raila alisema kuhusu zawadi zake kwa Mama Ida.

Raila alikuwa kwenye mahojiano hayo na marafiki wake ambao walifurahia 'trip' yake akiwa dereva wao ndani ya gari lake la kifahari.

Aidha alishambulia hasimu wake wa kisiasa naibu rais William Ruto na sera zake akisema haziwafai Wakenya.

"Sijui ni nani alifikiria mambo ya wheelbarrow akisema eti inaweza kuwasaidia Wakenya, hii mambo ya bottom up haieleweki," alisema Raila.

Alitetea ahadi yake ya kuzipa jamii maskini KSh 6K kila mwezi akisema ni mpango ambao umefikiria na kuhakikisha utafaulu.

Licha ya kuwa mkazi katika mtaa wa kifahari wa Karen, alisema mtaa wa Dagoreti huenda ungekuwa makao yake.

"Mimi nikiwa huko ndani nakula githeri na wakati mwingine nyama choma," aliongeza kiongozi huyo wa ODM.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke