Kiongozi wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Raila Odinga amezua wasiwasi kuhusiana na visa vya dhuluma ya kijinsia kuongezeka nchini.
Raila alisikitishwa na baadhi ya wapenzi ambao badala ya kukuza penzi lao hugeuka na kuwaua wenzao.
Kupitia kitandazi chake cha Twitter siku ya Jumanne, Aprili 20, Raila alisema endapo wapenzi wanashindwa kutatua tofauti zao, ni vyema kutengana na kuachia wenzao uhai wao.
"Ni jambo la kusikitisha kuwa baada ya kuteka moyo wa mwenzako, badala ya kuwapenda na kuwaenzi, baadhi hugeuka kuwa vita na wakati mwingine kifo. Endapo hamuwezi kusameheana, basi tenganeni na muwache uhai," Raila.