Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila afichua mipango ya kuunda muungano wa kumkabili DP Ruto

1f214233a5544696 Raila afichua mipango ya kuunda muungano wa kumkabili DP Ruto

Sun, 27 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila alisema wapinzani wake wajiandae kwa wimbi ambalo litafagia wengi 2022Ujumbe wake ulimlenga naibu rais huku akitupilia mbali sera zake za kubadilisha mfumo wa kiuchumi nchiniRaila anajulikana sana kutokana na wimbi la 2002 ambalo liliondoa KANU mamlakaniKinara wa ODM Raila Odinga Jumamosi Juni 26 alifichua kuna mipango inaendelea ya kuunda muungano mkubwa wa kisiasa.

Akiongea wakati wa mazishi ya Jakoyo Midiwo Gem, Raila alisema muungano huo utazua wimbi la kisiasa kwenye kivumbi cha 2022.

Raila alisema kikosi anachounda kitakuwa na wimbi ambalo litawabeba wapinzani wao na kuwazika kwenye kaburi la sahau.

"Nataka niwaambie kuwa tunaunda kikosi kikubwa. Wapinzani wetu hawajui kinachowasubiri. Wimbi linakuja. Nawaomba nyinyi wafuasi wetu mniamini kwa sababu najua tunapoelekea," alisema Baba.



Raila alimshambulia Naibu Rais William Ruto akisema wimbi hilo litamaliza siasa zake kuhusu kubadilishwa kwa mfumo wa kiuchumi.

"Ahadi za uchumi wa kuanzia kwa mwananchi kuenda juu inafaa kutupwa kwenye jaa la takataka. Hakuna kitu kama hicho, toroli na mikokoteni zitawasaidia na nini?" Raila alisema.

DP Ruto amekuwa akihubiri siasa za kubadili mfumo wa uchumi nchini akisema hio ndiyo suluhu ya masaibu yanayowakabili Wakenya.

Ni wazi kuwa wapinzani wake wamejihami vilivyo kukabiliana naye 2022 ambapo sera zake zimekuwa kuhusu mwananchi mlala hoi.

Matamshi ya Raila yalijiri wakati ambapo duru zinaarifu kuna mpango wa chama cha Jubilee kuungana na ODM ili kufanya kazi pamoja 2022.

Wandani wa Rais Kenyatta na wale wa ODM wamekuwa wakifanya vikao ili kuunda mwafaka wa jinsi vyama hivyo viwili vinaweza kuungana.

Aidha Raila pia amekuwa akiwarai waliokuwa wenzake kwenye muungano wa NASA, Kalonzo Musyoka, Musalia Mudavadi na Moses Wetangula kufufua muungano wao.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke