Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila aahidi kumaliza matapeli na kuinua biashara ya Mahindi

Ce6434c699386fd4 Raila aahidi kumaliza matapeli na kuinua biashara ya Mahindi

Sat, 20 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga amesema kwamba ni lazima wakulima wa mahindi kaunti ya Trans Nzoia wasaidiwe ili wafaidike kutokana na mazao yao.

Raila amesema wakulima wanafinyiliwa chini sana na viongozi wao ambao wanataka kujinufaisha wenyewe. Kulingana na Raila, eneo hilo limejaa viongozi walafi ambao huwachanganya wakulima na kuwashauri kuuza mahindi kwa bei ya chini alafu baadaye wao kuuza kwa bei ghali.

Raila ameahidi kuboresha na kuinua sekta ya ukulima wa mahindi na kila mkulima atafaidika pindi atakapoingia madarakani.

Akiwahutubia wakazi wa eneo la Trans Nzoia Jumamosi, Novemba 20, Raila alisema wakulima wana kibarua kigumu kudhibitisha kwamba wanafanya juhudi ya kupanda mahindi mengi nchini.

Kulingana na Raila, eneo hilo limejaa viongozi walafi ambao huwachanganya wakulima na kuwashauri kuuza mahindi kwa bei ya chini alafu baadaye wao kuuza kwa bei ghali.

"Kila mahali ulimwengu mzima hata ukienda Marekani, ama Ulaya, ukulima ni biashara bora zaidi. Serikali inafanya ukulima ili wananchi wawe na chakula ya kutosha kwa bei nafuu, tutafanya haya kwa wakulima wetu, ili wakulima waweze kupata haki yao kulingana na jasho yao,” Alisema Raila.

Raila pia alisema kwamba bei ya mbegu na mbolea itapunguzwa pindi atakapoingia madarakani.

Kinara huyo wa chama cha ODM alikuwa ameandamana na gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya na mwenzake wa Elgeyo Marakwet Alex Tolgos.

Akiwahubia wakazi wa Trans Nzoia, Raila alisema iwapo atakuwa Rais baada ya uchaguzi wa 2022, atahakikisha kwamba kila Mkenya anapata bima ya afya na kulipa KSh 6,000 kwa familia ambazo hazijiwezi kila mwezi.

Raila yuko katika ziara ya kuuza kauli mbiu yake ya "AzimiolaUmoja" kaunti ya Trans Nzoia huku akiwa na matumaini ya kunyakua kiti cha urais ingawa hajatangaza rasmi iwapo atakuwa debeni.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke