Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila Odinga: Nitakuwa Rais bila usaidizi wa Uhuru, Wakenya wataamua

7ac45ff87ab39a6f Raila Odinga: Nitakuwa Rais bila usaidizi wa Uhuru, Wakenya wataamua

Sun, 20 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga amesema atawategemea Wakenya wamchugue kuwa Rais wa tano iwapo atagombea kiti hicho 2020Wapinzani wa Raila walikuwa wamedai kwamba, anasubiri kuungwa mkono na Rais Uhuru Kenyatta ambaye muhula wake unakamilika mwaka ujaoHaya yanajiri baada ya Uhuru kutangaza kwamba yuko tayari kumuunga mkono mmoja wa vinara wa muungano wa NASA endapo wataafikiana kufanya kazi kwa pamojaKinara wa chama cha ODM Raila Odinga amefutilia mbali madai kwamba Rais Uhuru Kenyatta atamuunga mkono katika uchaguzi mkuu wa urais mwaka wa 2022.

Akizungumza kwenye mahojiano na Tanzania Star TV Jumamosi Juni 19, Raila alisema hamtegemei Uhuru kuingia Ikulu ila uamuzi wote unatokana na Wakenya.

Raila alisema Uhuru hana jukumu lolote la kuamua ni nani atakayemrithi muhula wake ukikamilika.

"Kama nataka kuwa Rais, sitahitaji Uhuru kunisaidia wala kuniunga mkono, hiyo ni uamuzi unaostali kufanywa na Wakenya, Uhuru hawezi akaniidhinisha mimi. Madai hayo ni propaganda tupu.," Raila Alisema.

Tangu salamu za handisheki mwaka wa 2018, Uhuru na Raila wamekuwa wakiafikiana kwa mambo kadha wa kadhaa na kupelekea baadhi ya Wakenya kubashiri kuwa Uhuru atamvulia koti kinara huyo wa ODM.

Kulingana na wapinzani wake, Raila amekuwa akipigia debe mpango wa BBI kwa manufaa yake ikiwemo uzinduzi wa nyadhifa mpya.

Raila pia alifutilia mbali madai kwamba chama chake kimo katika serikali ya Uhuru kama inavyodaiwa na baadhi ya wapinzani wake.

Haya yanajiri baada ya Uhuru kudai kwamba yuko tayari kumuunga mkono mmoja wa vinara wa muungano wa NASA.

Uhuru aliyasema haya alipofanya mkutano katika Ikulu ya Nairobi na viongozi kutoka Ukambani wiki jana.

Madai hayo yaliibua hisia mseto kutoka kambi ya naibu Rais William Ruto ambao walikashifu Uhuru kwa kuwatema waliofanikisha siasa zake za mwaka wa 2013 na 2017.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke