Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila Akutana na Familia ya Ayimba, Wafanya Maombi Kumtakia Nafuu

879c8d9f34ca5d50 Raila Akutana na Familia ya Ayimba, Wafanya Maombi Kumtakia Nafuu

Sun, 11 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ayimba alilazwa hospitalini baada ya kuugua ugonjwa wa malaria ya ubongo

- Familia yake imekuwa ikiomba usaidizi ili kulipa bili ya hospitali iliyofikia zaidi ya KSh 2M

- Raila alisema alikutana na familia yake kuwapa maombi na kuwahakikishia baba yao atapona

Kinara wa ODM Rala Odinga Jumapili Aprili 11 alifanya kikao na familia ya aliyekuwa kocha wa timu ya raga nchini Benjamin Ayimba.

Kupitia kwa taarifa iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa Facebook, Raila alisema alikutana na familia hiyo kuwaombea kipindi hiki wanapitia magumu baada ya mpendwa wao kuugua.

Ayimba aliripotiwa kuwa katika hali mbaya kufuatia kugunduliwa kuwa na ugonjwa wa malaria ya ubongo.

"Nimekutana na familia ya aliyekuwa kocha ya timu ya raga nchini Benjamin Ayimba ambaye kwa sasa amelazwa hospitali ili kuwaombea, kuwapa moyo na hata usaidizi," aliandika Baba kwenye Facebook.



Kulingana na The Standard ambalo lilinukuu vyanzo vya habari hii kutoka kwa familia, Ayimba kwa sasa amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (HDU) katika Nairobi Hospital, na hawezi kuzungumza au kumtambua mtu yeyote tokea siku kadhaa zilizopita.

"Haya yote wakati tumejaribu kudumisha faragha na hadhi yake lakini imefikia mahali ambapo hatuwezi kukaa kimya tena," familia iliiambia The Standard.

Waliomba msaada kulipia bili ya hospitali ambapo iliripotiwa kuwa zaidi ya milioni mbili.

“Familia ilidhani haingekuwa mbaya sana. Kwa hivyo, hatukutaka kuzua wasiwasi lakini wapi tumefika hapa sasa, tunatoa wito kwa wahisani wote nchi nzima kutusaidia," alisema mmoja wa wanao.

"Kwa kuwa bili ya hospitali sasa ni zaidi ya Sh2.2 milioni, tunahitaji msaada kwani tumemaliza rasilimali za familia," akaongeza.

Rais Uhuru Kenyatta tayari ametoa mchango wa KSh 1M ili kusaidia kulipa bili hiyo katika hospitali ya Nairobi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke