Watu wawili wamekamatwa nchini Nigeria kwa madai ya kutaka kumlawiti mtoto wa shule kutoka Australia ambaye alijiua.
Polisi wa Australia wanasema kuwa kijana aliyeathiriwa alikuwa ameuza picha chafu kwa mtu mtandaoni kabla ya kuanza kutoa vitisho na kudai pesa.
Baada ya uchunguzi wa kimataifa, wawili hao wanaodaiwa kuhusika walifuatiliwa hadi wakapatikana nchini Nigeria, ambapo watafikishwa mahakamani.
Polisi wanasema unyanyasaji wa kingono - haswa wa vijana - unaongezeka sana.
Maelezo ya umri wa mvulana huyo au alikoishi New South Wales hayajatolewa hadharani ili kulinda faragha ya familia yake.
Polisi wa New South Wales waliwataja wanaodaiwa kuwa wanyang'anyi kama "vijana wa kiume" na walisema walitishia kutuma picha kwa marafiki na familia ya kijana huyo ikiwa hatawalipa A$500 (£260; $330).
"Ujumbe huo ni wa kutisha. Una uzito sana na kuweka shinikizo kubwa kwa kijana huyo kulipa pesa," kamanda wa uhalifu wa mtandao wa jeshi la polisi, Matthew Craft, aliliambia gazeti la Sydney Morning Herald (SMH).