Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raia nane wafariki dunia katika shambulio mashariki mwa Congo

Uganda Iko Kwenye Tahadhari Wanamgambo Wa ADF Kuvuka Mpaka Kutoka DR Congo Raia nane wafariki dunia katika shambulio mashariki mwa Congo

Fri, 10 May 2024 Chanzo: Bbc

Takriban raia wanane walifariki dunia Alhamisi katika shambulio dhidi ya kituo kimoja cha afya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vilivyowanukuu wenyeji.

Shambulio hilo lilitokea katika jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo. Wenyeji walisema shambulio hilo lilitokana na wanamgambo wa Allied Democratic Forces, ambao waliahidi uaminifu kwa kundi la Islamic State mwaka 2019.

Kwa sasa tuna idadi ya waliofariki dunia, ikiwa ni pamoja na wagonjwa na mhasibu katika kituo cha afya, kiongozi wa jumuiya ya kiraia katika eneo la Beni Omar Kalisia aliwaambia waandishi wa habari. Kalisia aliongeza kuwa muuguzi mmoja hakuwepo, na nyumba moja ilichomwa moto.

Shambulio hilo la Alhamisi kwenye kituo hicho cha afya linafuatia shambulio la Mei 3 kwenye kambi ya watu waliokimbia makazi yao katika jimbo hilo hilo, na shambulio la Mei 7 katika kijiji kimoja katika jimbo jirani.

Mwishoni mwa 2021, DRC na nchi jirani ya Uganda zilianzisha operesheni ya pamoja ya kijeshi dhidi ya Allied Democratic Forces. Hadi sasa, jitihada hizo hazijafanikiwa.

Chanzo: Bbc