Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rafiki yake DP Ruto azungumzia unadaiwa mgawanyiko katika Chama cha ODM

9b9e2566b4c87c5a Rafiki yake DP Ruto azungumzia unadaiwa mgawanyiko katika Chama cha ODM

Mon, 3 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Murkomen anasema mgawanyiko huo ni kati ya pande mbili, upande mmoja unaotetea demokrasia, haki za binadamu na utawala bora na pande wa pili ambao unajumuisha wakala na wafanyabiashara wanaopenda kula zabuni

- Kulingana naye mvutano ni kati ya upande unaoongozwa na Seneta James Orengo, Otiende Amollo na Millie Odhiambo na upande mwingine unaongozwa na Junet Mohamed, John Mbadi na Gladys Wanga

- Seneta huyo wa Elgeyo Marakwet alibaini kuwa vikundi hivi viwili ndani ya chama cha ODM vyote vinamwamini Raila Odinga, lakini Odinga mwenyewe anaamini Pesa

Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen hatimaye ametoa kauli yake kuhusiana na unaodaiwa kuwa mgawanyiko ndani ya chama cha Orange Democratic Movement.

Kulingana na Murkomen, mgawanyiko huo ni kati ya pande mbili, upande mmoja unaotetea demokrasia, haki za binadamu na utawala bora unaoongozwa na Seneta James Orengo, Otiende Amollo na Millie Odhiambo.

Upande wa pili ambao unajumuisha wakala na wafanyabiashara wanaopenda kula zabuni unaongozwa na Junet Mohamed, John Mbadi na Gladys Wanga, na kufanya mgawanyiko kuwa vita kati ya watu bora na wafanyabiashara.

Seneta huyo wa Elgeyo Marakwet alibaini kuwa vikundi hivi viwili ndani ya chama cha ODM vyote vinamwamini Raila Odinga, lakini Odinga mwenyewe anaamini Pesa.

Aliongeza kuwa mrengo unaoongozwa na Junet, Mbadi na Wanga unataka mswada wa Mchakato wa Salamu ya Maridhiano upitishwe kama Serikali inataka.

"Mgogoro ndani ya ODM ni demokrasia kati ya haki za binadamu na mrengo wa utawala bora ukiongozwa na Orengo / Otiende / Millie dhidi ya wafanyabiashara na walaji zabuni wakiongozwa na Junet / Mbadi / Wanga. Wafanyabiashara dhidi ya Watu wenye maono. Wote hao wanamwamini Baba lakini Baba anaamini Pesa. Wafanyabiashara wanataka BBI ipite vile Serikali inavyotaka,” Murkomen aliandika kupitia Twitter.

Moses Kuria

Maneno yake yalijiri siku chache baada ya Mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria kujitolea kumsaidia kiongozi wa ODM Raila Odinga kutatua mgawanyiko unaodaiwa kuwa ndani ya chama cha Orange.

“Mpendwa rafiki yangu Raila Odinga. Ni wazi sasa tuna ODM inayoongozwa na Junet, Mbadi & Opiyo Wandayi na ODM Asili inayoongozwa na Orengo, Otiende Amollo na Okongo Omogeni. Ikiwa unahitaji msaada kutatua shida hii unayo nambari yangu,” Kuria alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke