Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RUTO: Nilimfanya Kenyatta kuwa Rais wa Kenya

Uhuru Na Ruto Nilimfanya Kenyatta kuwa Rais wa Kenya

Wed, 6 Jul 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Akizungumza mjini Meru katika siku ya mwisho ya ziara yake ya Mlima Kenya Mashariki, Makamu wa Rais Ruto amesema wakati Mahakama kuu, ilipoamuru uchaguzi wa marudio mnamo 2017, Rais Kenyatta hakutaka kurudia na alimlazimisha kurudia uchaguzi huo kwani asingemruhusu kuacha kazi aliyoifanya kwa kuwa aliamka saa 10 alfajiri kufanya mikutano ya kampeni

“Kuna watu ambao wanasambaza rekodi fulani wakidai nilimlazimisha Uhuru kugombea. Wacha niwaambie kwamba hawajui jinsi tulivyomfanya Uhuru Kenyatta kuwa rais. Sisi ndio tuliofanya kazi kwa bidii kuhakikisha tumeshinda”,alisema Dkt. Ruto

Mashambulio yanayoendelea dhidi ya Rais kutoka kwa naibu wake yanadaiwa kuchochewa na rekodi ya sauti iliyovuja ambapo Dkt Ruto anasikika akiwaambia wajumbe wa Gikuyu Rais alikuwa amejitoa baada ya kubatilishwa kwa kuchaguliwa kwake tena na Mahakama ya Juu mwaka 2017

Chanzo: www.tanzaniaweb.live