Naibu kamanda wa Kikosi cha (RSF), nchini Sudan Abdel Rahim Hamdan Daglo, anasema kundi lake litaendelea kusonga mbele na kuchukua majimbo yaliyosalia nchini humo kutoka kwa jeshi.
Tamko la Bw Daglo lilikuja baada ya hivi karibuni RSF kupata mafanikio katika uwanja wa vita katika eneo la magharibi la Darfur, ambako iliteka baadhi ya majimbo na kambi za jeshi.
Darfur inachukuliwa kuwa ngome ya RSF.
"Tutaelekea katika majimbo mengine yaliyosalia na makao makuu ya [jeshi], na yatakuwa chini ya udhibiti wetu, Mungu akipenda," Bw Daglo alisema siku ya Alhamisi alipokuwa akiwahutubia wapiganaji wa RSF waliokuwa na furaha katika mji mkuu wa jimbo la Darfur la Kati la Zalingei.
Hapo awali, wanajeshi walipuuza mafanikio ya uwanja wa vita yaliyopatikana hivi majuzi na kikundi huko Darfur.
Mazungumzo ya amani kati ya pande hizo mbili yanaendelea katika mji wa bandari wa Saudia wa Jeddah katika jitihada za kumaliza mzozo uliozuka katikati ya mwezi Aprili.