Tue, 17 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiongozi wa chama cha Roots Profesa George Wajackoyah sasa anaitaka serikali kuwatengea likizo ya kila wiki waumini wa dini ya Kiislamu.
Kwa mujibu wa Profesa Wajackoyah, waumini wa dini zingine wana likizo kwa ajili ya siku zao za ibada na kupumzika huku Waislamu wakiwa hawana siku yoyote ile.
"Ninataka serikali kutenga Ijumaa kuwa likizo kwa Waislamu. Wanasabato wana Jumamosi na Wakristo wana Jumapili lakini Waislamu hawana siku yao," Wajackoyah amesema.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live