Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Profesa Hammo Apuuza Jemtai, asema anawatunza wanawe kikamilifu

E66ecfca9f4b816c Profesa Hammo Apuuza Jemtai, asema anawatunza wanawe kikamilifu

Sun, 2 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

MchekeshajiHerman Kago , maarufu kama Profesa Hammo, amekanusha madai kuwa amehepa majukumu ya ulezi baada ya kuwa kwenye uhusiano na msanii mwenzake Jemtai.

Hammo amehjitetea baada ya Stella Jemutai Koitie maarufu kama Jemtai kudai kuwa alimhepa baada ya wao kubarikiwa na watoto wawili.

Jemtai alisema walikutana kwenye Churchill Show na mapenzi yakamea ambapo walishiriki penzi na kujaliwa na watoto wawili.

Hata hivyo, alisema Hammo alimhepa mwaka wa 2020 na licha ya kuwa sauti nzito kwenye mojawapo wa vituo vya redio humu nchini hajakuwa akitunza familia yake.

Habari Nyingine: DP Ruto Akaidi Ushauri wa Rais Uhuru, Aingia Kwake Bila Kubisha

Hata hivyo Hammo alisema yeye ni ndume muungwana na amaekuwa akitekeleza majuku yake kama baba wa watoto wake.

"Niko na watoto ambao wanaishi na mimi na wengine ambao hawaishi na mimi. Lakini nimekuwa nikitekeleza majukumu kwa watoto wangu kuanzia siku ya kwanza na hakuna siku wamekuwa hawana chakula au chochote wanachohitaji," alisema

Hammo alisema mkewe ndiye hutoa usaidizi kwa watoto wa msanii Jemutai kama walivyokubaliana.

"Mke wangu ndiye hutuma usaidizi kwa watoto ambao hatuishi na wao. Hii ni baada ya sisi kuelewana hivyo kati ya familia yangu na mama wa watoto hao (Jemutai)," aliandika kwenye Facebook Jumapili Mei 2.

Hammo alisema matusi ambayo yamekuwa kwenye mtandao tanguJemtai afichue hayo yanawaathiri wanawe shuleni pakubwa.

Aidha alidai kuwa huenda Jemtai amepata magumu maishani ambayo yamemfanya kuwa na machungu.

"Wakati nmwingine maishani watu huhangaika baada ya kukosa kupata walivyokuwa wametarajia baada ya changamoto kuibuka.Nimekuwa nikitekeleza wajibu wangu kama baba kwa watoto wangu na nitaendelea kufanya akzi kwa bidii ili kuwatunza," alisema Hammo.

Hammo alijipata pabaya baada ya Jemtai kufichua kuhusu maisha yake ya siri na wanamtandao wamekuwa wakimlima vikali.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke