Tue, 14 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Polisi nchini Sudani wamelazimika kutumia Mabomu ya Machozi kutawanya Waandamanaji waliokusanyika karibu na Makazi ya Rais Jijini Khartoum, wakipinga Makubaliano yaliyomrejesha Waziri Mkuu, Abdalla Hamdok Madarakani.
Wanaharakati na Makundi mbalimbali ya Kidemokrasia bado yanasisitiza Jeshi halipaswi kuwa sehemu ya Serikali kwani haliwezi kuaminiwa kuongoza Nchi kuwa ya Kidemokrasia
Tangu Mapinduzi kufanyika Oktoba 25, watu wapatao 50 wameripotiwa kupoteza maisha huku mamia wakijeruhiwa Jenerali Abdel Fattah al-Burhan mara baada ya kumrejesha Hamdok aliahidi Uchaguzi Mkuu Julai 2023.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live