Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, ametuma picha ya polisi na jeshi wakionekana nje ya nyumba yake kabla ya kampeni za uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika katika wilaya ya Kayunga.
Rais Yoweri Museveni anatarajiwa kutembelea katika wilaya ya Kayunga kumfanyia kampeni mgombea wa chama tawala anayewania nafasi ya uenyekiti.
Uchaguzi huo mdogo umepangwa kufanyika Alhamisi na chama tawala na upinzani kwa pamoja vinataka kuonyesha uwezo wao katika eneo hilo.
Bobi Wine ameshutumu jeshi na polisi kwa kujaribu kumzuwia kuondoka nyumbani kwake :
This morning, ahead of my planned visit to Kayunga District to campaign for our flag bearer, the police and military deployed overnight around my home in an apparent attempt to block me from leaving. The cowardly regime is on its way out. A matter of time.#WeAreRemovingADictator pic.twitter.com/Iopz14Uwoq
— BOBI WINE (@HEBobiwine) December 14, 2021