Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi wapata mwil anayedaiwa kumuua mwanahabari wa BBC

5c59ed6f679bee22 Polisi wapata mwil anayedaiwa kumuua mwanahabari wa BBC

Mon, 22 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Madai mapya yameibuka kuhusiana na kifo cha mwanahabari wa shirika la utangazaji BBC Kate Mitchell kilichotokea siku ya Ijumaa, Novemba 19 kwenye chumba cha hoteli moja jijini Nairobi.

Mshukiwa anadaiwa kujitoa uhai kwa kujirusha chini kutoka orofa ya nane ya chumba walimokuwa na mwanahabari huyo.

Maafisa wa upelelezi wanaamini kwamba mwanahabari wa BBC Kate Mitchell aliuawa na mwanaume ambaye alionekana naye dakika ya mwisho kabla kifo chake. Kate na mwanamume huyo wanasemekana kugombana na kumlazimu mwanahabari huyo kuitisha usaididizi lakini aliuawa kabla ya kusaidiwa.

Maafisa wa upelelezi sasa wanaamini kwamba Mitchell aliuawa kwa kunyongwa na mwanaume ambaye alikuwa naye chumbani siku hiyo.

Kwa mujibu wa taarfia za Citizen TV, Mitchell aliitisha usaidizi kwa kugonga kengele baada ya ugomvu kuzuka baini yake na mwanaume huyo lakini hakuna mtu alienda kumsaidia.

Afisa mkuu wa polisi jijini Nairobi Benjamin Nthumbi alidhibitisha kisa hicho akisema mlango wa chumba cha Kate ulikuwa umefungwa na ndani wakati alifika katika eneo la tukio.

Nthumbi alisema maafisa wanaochunguza kisa hicho walipata dirisha la chumba hicho likiwa limevunjwa na kuona mwili wa mwanaume ukiwa sakafuni.

Imedaiwa kwamba, mwanaume huyo alijitoa uhai kwa kujirusha kutoka orofa ya nane baada ya kumuua Kate.

"Baada ya kuangali chini kupitia dirishani, maafisa wa upelelezi waliona mwili wa mwanaume ukiwa sakafuni, iligunduliwa baadaye kwamba alikuwa na Kate chumbani," Nthumbi alisema.

Hata hivyo uchunguzi kuhusiana na kifo chake umeanzishwa huku shirika la BBC likifutilia mbali madai kwamba huenda aliangamizwa kwa ajili ya kikazi.

" Nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wetu Kate Mitchell. Alifariki dunia akiwa jijini Nairobi kwenye chumba cha hoteli," Sehemu ya tangazo hilo kama ilivyonukuliwa.

" Chanzo cha kifo cha Kate hakijabaini lakini tunashirikiana na ubalozi wa Uingereza na polisi jijini Nairobi kufanya uchunguzi. Tutapeana usaidizi kadri ya uwezo wetu kwa wapepelezi na kile tunachokijua, hakuna ishara kwamba kifo chake kilitokana na majukumu yake kama mfanyakazi wa BBC," Taarifa zaidi ilisoma.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke