Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi wamnasa jamaa kufuatia kifo cha mwanariadha mwingine

1e6f18eda7f20647 Polisi wamnasa jamaa kufuatia kifo cha mwanariadha mwingine

Thu, 14 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Siku moja tu baada ya kifo cha nyota mashuhuri wa mbio za nyika wa Kenya Agnes Tirop, mwanariadha mwingine ameripotiwa kufariki dunia katika kaunti ya Kirinyaga.

Kennedy Nyamu alishtakiwa kwa kumkata kisogoni Muthoni katika kijiji cha Kianjege Mashariki huko Kerugoya baada ya mzozo wa kinyumbani.

Kulingana na dadake Muthoni, Jane Nyawira King’uru, mshtakiwa alimshambulia baada ya kumpkonya simu na kuipitia

Polisi huko Kerugoya, wamemkamata jamaa mmoja kwa tuhuma za kumuua mpenziwe, Edith Muthoni, 27, Jumanne usiku, Oktoba 12.

Kennedy Nyamu alishtakiwa kwa kumkata kisogoni Muthoni katika kijiji cha Kianjege Mashariki huko Kerugoya baada ya mzozo wa kinyumbani.

Kulingana na dadake Muthoni, Jane Nyawira King’uru, mshtakiwa alimshambulia baada ya kumpkonya simu na kuipitia.

“Wawili hao walichumbiana kwa miaka mitatu. Siku ya tukio walianza kuzozania simu ya Muthoni," Nyawira alisema kulingana alivyonukuliwa na The Standard.

Muthoni anajulikana kwa uhodari wake katika mbio za mitaani. Alifanya kazi pia kama skauti katika Huduma ya Wanyamapori (KWS) katika Kaunti ya Embu.

Alipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kerugoya akiwa katika hali mbaya. Hata hivyo alaiga dunia akipokea matibu.

Norman Gitari, msimamizi mkuu wa Hospitali ya Kerugoya, alibaini kuwa Muthoni alikuwa ameletwa hospitalini humo na msamaria mwema.

Kulingana na taarifa ya Jumatano, Oktoba 14 kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), mtuhumiwa huyo aliandamana na polisi hadi eneo la tukio.

Jane Nyawira alisema dadake alikuwa mtulivu ambaye angefungua moyo wake wakati mambo yameshindikana.

Alidokeza kwamba dadake alionyesha ari ya kupenda riadha akiwa angali mchanga.

Jane alifichua kuwa alipata habari akiwa kazini kuwa dadake amepelekwa hospitalini.

“Jumanne, nikiwa kazini, nilipokea simu kutoka kwamba Muthoni alikuwa amepelekwa katika Hospitali ya Kerugoya akiwa katika hali mbaya. Nilikimbilia huko na nikaambiwa amelazwa katika wodi ya wagonjwa mahututia. Muda mfupi baada ya kupata wodi aliyokuwa amelazwa wauguzi waliniarifu kwamba alikuwa amekata roho,”Jane alisimulia kwa uchungu.

Babake Muthoni amewataka polisi kufanya uchunguzi wa kina na kuhakikisha kuwa wahusuka wa mauaji ya mwanawe wanatiwa mbaroni.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke