Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi taabani baada ya mwalimu kufariki kwenye seli Migori

9783f3da13c2021e Polisi taabani baada ya mwalimu kufariki kwenye seli Migori

Mon, 5 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Henry Wanga Aura alikamatwa Ijumaa, Aprili 1, baada ya kuvurugana na mke wake

- Aura alifariki Jumamosi, Aprili 3, asubuhi akiwa amezuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Ratanga

- Wakazi wa kijiji cha Ratanga walivamia kituo hicho cha polisi wakitaka kujua chanzo cha kifo cha mwalimu huyo

- Mwili wa Aura ulipelekwa katika hifadhi ya kaunti ya Migori ambapo upasuaji unasubiriwa

Afisa mmoja wa polisi katika Kituo cha Polisi cha Ragana, kaunti ya Migori amemulikwa na wakazi kufuatia kifo cha mwalimu ambaye alikuwa katika seli yake.

Henry Wanga Aura ambaye n mwalimu wa shule ya msingi alikamatwa Ijumaa, Aprili 1, baada ya kuvurugana na mke wake

Wakazi wa kijiji cha Ratanga walivamia kituo hicho cha polisi wakitaka kujua chanzo cha kifo cha mwalimu huyo wengi wakidai kuwa kuna jambo ambalo lilimfanya Aura kujitia kitanzi.

Kulingana na mama yake marehemu, Rosenael Aura, mwalimu huyo alipatikana amefariki siku ya Jumamosi, Aprili 3, katika seli ya polisi alimokuwa amezuiliwa.

“Alizozana na mke wake. Nilikuwa kwangu na nilimsikia mke wake akipiga kelele.Hakuna mtu ambaye alikuwa anataka kuelezea kilichokuwa kimetokea kwa hivyo niliona ni mzozo wa kawaida wa kifamilia," alisema mama Aura.

Mama huyo alisema aligundua kifo cha kwa mwanawe wakati alimpelekea chakula siku ya tukio hilo.

“Nilimpelekea kiamsha kinywa lakini polisi aliyekuwa kwenye zamu alikuwa ananizuia kumuona. Nilikuwa na shauku na hivyo niliwaita kaka zake na ndipo tuliambiwa alikuwa amefariki. Afisa alisema alijitia kitanzi akitumia shati usiku uliotangulia," aliongezea.

Mke wa marehemu alikuwa amewasilisha kesi ya kupigwa na hivyo kupelekea kukamatwa kwa Aura. Alitoroka baada ya kugundua mume wake amefariki.

Wakazi walizua malalamishi ya mauji ya kiholela ya polisi katika kituo hicho kipya cha Ragana.

Pappine Odongo alisema maafsa katika kituo hicho hutumia nguvu kupita kiasi wakati wanawakabili washukiwa akiongezea kuwa huenda kifo cha Aura kilitokana na mateso.

Kamanda wa polisi wa Suna Magharibi, Wilson Nduati alizuru eneo la tukio akiahidi uchunguzi kuhusu kisa hicho utafanywa.

Mwili wa Aura ulipelekwa katika hifadhi ya kaunti ya Migori ambapo upasuaji unasubiriwa.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke