Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi: "Ni ngumu kuwakamata wanasiasa wanaokiuka sheria za COVID-19"

B7684890f95ea6ea Polisi: "Ni ngumu kuwakamata wanasiasa wanaokiuka sheria za COVID-19"

Tue, 19 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Msemaji wa polisi Bruno Shioso amekiri kwamba kuwakamata wanasiasa musimu huu wa COVID- 19 imekuwa vigumu sana. Shioso alisema polisi wamekuwa wakipiga marufuku mikusanyiko mikubwa na mikutano ya kisiasa lakini yote hayazingatiwi.

Kulingana na Shioso, polisi hukubaliwa kuwakamata wanasiasa kufuatia kanunu kadhaa ambazo lazima wazingatieMsemaji wa polisi Bruno Shioso amekiri kwamba ni vigumu sana kuwakamata wanasiasa ambao wanafanya mikutano ya kisiasa licha ya kupigwa marufuku musimu huu wa mlipuko wa virusi vya COVID-19.

Shioso alisema ikija kwa siasa kuna mbambo mawili tofauti, kuzuia uhalifu na kulinda sheria.

"Kitu cha kwanza muhimu ni kuzuia uhalifu na hii kwa mara nyingi kuangazia wananchi. Kwa usalama wao tumewaambia mara kwa mara wasiwe wakihudhuria mikutano ya kisiasa lakini hawasikii, iwapo tutaangazia na kukabiliana na uhalifu, basi hakuna mwanasiasa atakaye andaa mikutano hii ya kisiasia,"Alisema Shioso.

Akiwa kwenye mahojiano na runinga ya Citizen siku ya Jumatatu, Oktoba 18, Shioso alisema idara ya polisi imekuwa ikijaribu sana kupiga marufuku mikutano ya kisisasa na mikusanyiko mikubwa bila mafanikio.

" Tumekuwa tukitoa taarifa kwa umma, lakini wakati mwingine mikutano imekuwa mingi, na hii inakuwa changamoto kwetu sisi kuidhibiti, kwa upande mwingine umati ukiwa mdogo itakuwa rahisi kwetu sisi kuwakamata watu wote,"Shioso aliongezea.

"Iwapo kuna mkutano wa kisisasa, yafaa tuwakamate wote watakaokuwa wamehudhuria lakini mara mingini umati huwa mkubwa sana kwa hivyo inakuwa changamoto kwetu sisi. "Aliongezea Shioso.

Shioso alisisitiza kwamba kukamata idadi kubwa ya wanaokiuka sheria ya COVID-19 ni ngumu sana na ndio wakati mwingine polisi hawashughuliki.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke