Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Piga Luku: Picha ya Wanawe DP Wakihakisha ameng'ara wakati wa harusi ya June

Efffcbb3247bf2a2 Piga Luku: Picha ya Wanawe DP Wakihakisha ameng'ara wakati wa harusi ya June

Fri, 28 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ilikuwa ndiyo siku kubwa maishani kwa June Ruto kama ilivyo kwa mwanamke yeyote ambaye hufika kilele kwa kuingia katika ndoa kupitia harusi

- Familia yake ilikuwepo kushuhudia June akiondoka kuana safari ya kula tunda la ndoa baada ya kusema 'I DO'

- Babake na kaka zake waliamua kupiga luku vilivyo ili kuendelea kufanya sherehe hiyo kufana kama ilivyopangwa

Familia ya Naibu Rais William Ruto Alhamisi Mei 28 ilihakikisha imepamba siku kubwa maishani mwa mmoja wao June Ruto vilivyo.

Walifanya kila namana kuhakikisha kuwa siku yake imefana kabisa alipokuwa akiingia katika ndoa na mchumba wake Alex Ezanagu.

Kuanzia yule mdogo hadi kwa DP, kila mmoja alihakikisha kuwa vazi lake linaongeza mwanga kwenye sherehe ya June.

Picha ya ndugu zake June wakiunda vazi la baba yao iliibuka kwenye mtandao na ni wazi kuwa hawakutaka 'achome picha'.

Ruto hajazoea mavazi ya aina aliyotakiwa kuvaa Alhamisi Mei 27 na hivyo kuanzia kwa kifungua mimba wake Nick Ruto waliamua 'kusaidia baba'.

DP alivalia suti nyeusi iliyoonekana ghali huku sharti lake nyeupe likifungwa tai ambayo ni maarufu na sherehe za mbwembwe.

Kichwani alivalia kofia aina ya Cow Boy na kisha akashikilia mkongojo na kuhakikisha anapiga luku ya 'Big man Bazuu'.

Habari Nyingine: Pongezi Sana! Ujumbe wa Rais Uhuru Kwa June Ruto Siku Yake Kubwa

Hata hivyo, sherehe hiyo ya June ilikosa mkono wa serikali baada ya Rais Uhuru Kenyatta kukosa kuhudhuria.

Rais alikuwa na shughuli kibao na kuahidi kuwa atafanya mpango kuonana na maharusi hao baada ya sherehe za Madaraka Dei kukamilika.

"Pongezi sana, nitawaona tukitoka huko Kisumu, eeh pongezi sana," Rais Kenyatta alimtuma DP kuenda kuwapasha June na mpenziwe Alex Ezanagu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Taama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke