Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha za Waziri Matiang'i Akilindwa na Kikosi Spesheli Zazua Gumzo

04fabe1fbca0aad6 Picha za Waziri Matiang'i Akilindwa na Kikosi Spesheli Zazua Gumzo

Sat, 11 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Maafisa waliokuwa wamejihami vikali waliandamana na waziri Fred Matiang'i kumlinda huko Laikipia IjumaaWanamtandao walitoa hisisa mseto wakisema kwelie Matiang'i ni 'Super CS' na anafurahia kikosi spesheliMatiang'i alionya kuwa atawafinya wanasiasa ambao wanachochea wakazi na kuzua mashambulizi Picha zimeibuka mtandaoni zinazoonyesha Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i akiwa na kikosi spesheli cha maafisa wa polisi.

Picha hiyo inaonyesha Matiang'i akilindwa vikali huku akitoa onyon kali kwa majangili ambao wamekuwa wakihangaisha wakazi Laikipia.

Matiang'i alisema serikali sasa iko imara kupambana na wezi wa mifugo ambao wamekuwa wakishambulia wakazi.

Alikuwa eneo hilo kukagua hali baada ya serikali kutuma kikosi spesheli ili kupambana na washambulizi ambao wanawakosesha amani wakazi.

Matiang'i alikuwa ameandamana na mshirikishi wa bonde la ufa George Natembeya na mamia ya maafisa wa polisi ambao serikali imesema watapiga kambi kaunti hiyo.

"Kuna hao ambao wanajifanya eti wao ni wabaya. Sasa wakuje wakutane na serikali, hakuna mchezo saa hii. Maafisa hawa spesheli watakuwa hapa wakifanya mazoezi ili wakutane na hao wanajifanya tuone," alisema Matiang'i.



Waziri alisema kuna wanasiasa ambao wanataka baadhi ya watu eneo hilo waondoke.

"Haya mambo yanafanywa wakati uchaguzi unakaribia. Nataka niwaambie viongozi wetu wa kisiasa kuwa hatutaruhusu hili. Mnasema eti unataka kufukuza watu wengine ili usajili wengine kama wapiga kura, tunajua." alisema Matiang'i.

Mbunge wa Tiaty William Kamket alikamatwa Jumatano Septemba 8, 2021 kuhusiana na machafuko hayo katika wadi ya Ol Moran kaunti ya Laikipia.

Kamket alikamatwa muda mfupi baada ya polisi kumkamata mbunge wa zamani wa ODM Matthew Lempurkel. Mwanasiasa huyo pia alikuwa amehusishwa na mapigano hayo.

Kamket hata hivyo aliachiliwa Ijumaa kwa dhamana ya KSh 500,000 pesa taslimu.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke