Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha za Rais Uhuru na Ruto Wakicheka pamoja zasisimua hisia za kisiasa

1a99bae2671b1912 Picha za Rais Uhuru na DP Wakicheka pamoja zasisimua hisia za kisiasa

Wed, 20 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Kenyatta na Naibu Rais Ruto wamekuwa hawapatani kisiasa kwa muda na Wakenya walisubiri kuona vile watatengamana wakati wa maadhimisho ya siku ya Mashujaa. Picha ya wawili hao wakitabasamu ilipopakiwa kwenye mitandao ilisambaa huku ikipokelewa kwa hisia mseto.

Sherehe za Mashujaa ilikuwa ishara tosha kuwa wanasiasa hujibizana tu kwenye runinga na mikutanoRais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wamesisimua mtandao baada ya kuonekana wakichangamka pamoja wakati wa sherehe za Mashujaa Kirinyaga.

Imekuwa muda tangu Wakenya kuwaona Rais na Ruto wakisemezana na hivyo picha zao zilipokelewa kwa hisia mseto.

DP Ruto aliamka alipokuwa ameketi na kufika kwa Rais ambapo walionekana wakisemezana kama marafiki wa karibu.

DP anaonekana akitabasamu huku akiwa ametoa barakoa ishara kwamba alichokuwa akimwambia Rais kilikuwa na ucheshi.

Baada ya kumalizana, DP anaondoka huku Rais akimtaka 'kugotta' ambayo huwa ni ishara ya watu wawili kuelewana kwa jambo fulani.

Awali, kinara wa ODM Raila Odinga ndiye alikuwa amepokea salamu tamu wakati Rais aliwasili katika jukwaa kusalimia wageni.

Wakati humu Rais alionekana kumsalimia DP kwa haraka na kusonga mbele bila hata kusemezana kwa lolote.

Lakini Rais alipofika kwa Raila, walisalimiana na kusemezana kwa sekunde chache na ilikuwa wazi salamu zao zilikuwa za marafiki.

Sherehe hizo zilionekana kuwa nafasi ya DP Ruto kukutana na mahasimu wake na akafaulu kutengamana na wao bila wasiwasi.

Awali, DP alifika kwenye jukwaa katika uwanja wa Wang'uru na kupokea salamu kutoka kwa viongozi waliokuwa wamefika mbele yake.

Walikuwa ni kinara wa ODM Raila Odinga, Gavana Ann Waiguru, Katibu wa Jubilee Raphael Tuju Seneta Gideon Moi, Musalia Mudavadi, Martha Karua baadhi ya wengine.

Licha ya hapo jana kumshambulia Raila akimuita prpject ya serikali katika uchaguzi wa urais 2022, wawili hao walisalimiana na kutabasamu huku wakipeana salamu kwa sekunde kadhaa.

DP pia alionekana kuwa na 'tete-a-tete' na Gavana wa Mombasa Hassan Joho huku wote wawili wakitabasamu.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke