Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha za Rais Uhuru, Waziri Borris wakipiga raundi na kufurahia stori

F9f0411847df3950 Picha za Rais Uhuru, Waziri Borris wakipiga raundi na kufurahia stori

Fri, 30 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Uhuru na Borris walionekana kwenye picha wakiwa na furaha kama marafiki wakuu waliokutana baada ya mudaNi wazi kuwa wawili hao walikuwa na wakati mzuri pamoja baada ya kuongoza kikapo ambapo KSh 400B zilichangwa kusaidia watoto maskini dunianiBaada ya kikao cha kuchangisha pesa, Borris aliamua kumtembeza Rais ili afurahie bustani na mandhari ya UingerezaKeyatta alitumia ziara hiyo pia kutafuta michuzi kutoka kwa wawekezaji wa UK ili kusaidia miradi yake ya maendeleo humu nchiniRais Uhuru Kenyatta amekuwa nchini Uingereza ambapo alihudhuria kikao cha washikadau kuhusu elimu.

Rais Kenyatta aliongoza kikao cha kushawishi mataifa kukubali kuchangia katika kufadhili elimu ya watoto maskini duniani.

Kenyatta aliungana na Waziri Mkuu wa Uingereza Borris Johnson kuongoza kikao hicho ambapo bilioni 400 zilichangwa na mataifa takriban 19.

Rais alionekana kuwa na wakati mzuri nchini humo huku urafiki wake na Borris ukionekana wazi kupitia mazungumzo yao na pia walivyochukua muda kubarizi pamoja.



Read also

Magazeti Alhamisi, Julai 29: Wabunge Kupitisha BBI Bila Rifarenda



Picha zilizochapishwa na Ikulu zilionyesha wawili hao wakiwa na furaha huku wakitembea kwenye bustani Uingereza.

Ukiwatazama, ni wazi kuwa wanapiga gumzo kama marafiki wawili wakuu ambao wamekaa bila kukutana.

Kwenye mojawapo wa video, Kenyatta anaskika akiporomosha kiingereza huku ulimi wake ukiskika kuchukua mkondo wa Uingereza.



Licha ya kuwa alizaliwa Ichaweri kaunti ya Kiambu, na kulelewa huku akifunzwa lugha ya mama ya Kikuyu, Kenyatta hutangamana vizuri viongozi wa uzunguni.

Alihudhuria chuo cha St Mary's ambapo asilimia kubwa ya walimu ilikuwa ni kutoka ng'ambo na hivyo wanafunzi wakafaulu kujifunzi msamiati wa maneno ya kiingereza.

Baada ya hapo alielekea Marekani ambapo alihudhuria chuo cha Amhest mjini Massachussets aliposomea masuala ya kisiasa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke