Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha za Kukumbukwa za Mama Sarah Akimkumbatia Rais wa Zamani Barrack Obama

35b9dd8ecefc5bfc Fahamu ni kwa nini Hayati Rais wa Tanzania John Magufuli alipewa jina Pombe

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Upendo uliokuwepo kati ya aliyekuwa rais wa 44 wa Marekani Barack Obama na Nyanyake Sarah Obama ulidhihirirshwa wazi kwenye picha kadhaa mitandaoni na bila shaka ulikuwa wa dhati.

Mama Sarah aliaga dunia Jumatatu Machi 29, 2021 akipokea matibabu katika hospitali ya Jaramogi Odinga, hadi kifo chake alikuwa na umri wa miaka 99.

Kwa mujibu wa kanuni za dini ya Kiislamu, Mama Sarah Obama atazikwa kesho ( Jumanne) nyumbani kwake eneo la Kogelo katika kaunti ya Siaya.

Mwanawe Marsat Obama, alisema mama Sarah 99, amekuwa akiugua kwa muda mrefu tangu mwezi Septemba mwaka jana alipopatwa na mshtuko wa moyo.

Mama Sarah alikuwa mke wa tatu wa Marehemu Hussein Onyango Obama, babuye Barack Obama aliyekuwa rais 44 wa Marekani.

Mwenda zake Sarah anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne Machi 30, kwake nyumbani Kogelo kaunti ya Siaya kulingana na kanuni zadini ya Kiislamu.

TUKO.co.ke inafahamu kwamba Obama alimtembelea mara ya mwisho marehemu mama Sara mwezi Juni mwaka wa 2018 alipokuwaa ziarani hapa Kenya.

Uhusiano kati ya Sarah Obama na Barack Obama ulikuwa wa kupigiwa mfano.

Kinara wa ODM Raila Odinga amemtaja Mama Sarah kama mtu aliyetumia uongozi wa Barack Obama Marekani kuchangia pakubwa masomo ya mtoto msichana na kupigana na maovu katika jamii.

Raila alimsifu marehemu kwa uweledi wake huku akiongeza kwamba Mama Sarah aliisha maisha ya kuona mbele jambo ambalo lilimuwezesha kulea familia yake licha yeye kuwa mjane.

Rais Uhuru Kenyatta naye ametaja Mama Sarah kama nguzo muhimu katika jamii na mtetezi wa haki, huku akisema kwamba mchango wake kwa taifa utakosekana.

Mama Obama awali alilazwa katika hospitali ya rufaa ya Siaya kabla ya kuhamishiwa hadi katika hospitali ya rufaa ya Jaramogi Oginga Odinga mjini Kisumu.

Mkurugenzi wa Afya katika kaunti ya Kisumu Biko Opidi alidinda kuelezea kilichomuua Mama Sarah, huku akisema kwamba kisheria sio vema kutangaza au kutoa habari za mgonjwa kwa umma kama mwenyewe au familia haijakubali.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke