Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha ya wananchi wasioshughulika na Rais Kenyatta yachangamsha Tangatanga

75ca2136bb9da080 Picha ya wananchi wasioshughulika na Rais Kenyatta yachangamsha Tangatanga

Tue, 27 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wananchi walionekana wakiendelea na shughuli zao bila msisimko wa ziara ya Rais

- Tangatanga walitumia picha hizo kuwarushia mishale wenzao wa Kieleweke mtandaoni

- Mirengo hiyo miwili imekuwa ikichapana kisiasa kwenye mitandao tangu DP Ruto na Rais watofautiane

Wafuasi wa Rais Uhuru Kenyatta na wale wa naibu wake William Ruto wanaendelea kulimana kisiasa kwenye mitandao huku ushindani wa 2022 ukikaribia.

Kila mrengo una makamanda kwenye mtandao ambapo wanakaa macho kushambulia mahasimu wao.

Hali ilikuwa kama hiyo Jumatatu wakati wa ziara ya Rais Kenyatta kaunti ya Nyeri baada ya picha moja kuibuka mtandaoni iliyoonyesha wananchi wasiokuwa na shughuli kwa Rais.

Rais alikuwa akielekea katika halfa iliyokuwa ikifanyika katika chu cha Dedan Kimathi wakati alizuru mradi wa barabara ya Kenol-Nyeri-Marua unaoendelea.



Tofauti na ilivyo kawaida ambapo wananchi hufurika eneo kumpungia mkono Rais, wakazi jana walionekana wakiendelea na shughuli zao kwenye picha hiyo.

Wakosoaji wa Rais walisema hiyo ni ishara kuwa wakazi wamechoka na uongozi wake na hivyo hawana la kusisimkia.

Wanatangatanga wamekuwa wakikosoa Rais kutokana na gharama ya maisha kuongezeka wakisema hilo limechangiwa na uongozi mbaya.

"Watu wa Nyeri kweli hawataki mchezo pia. Yaani hamtakai hata kujitokeza msalimie Rais," Eve Wambo aliandika kwenye picha hiyo ya Rais.

Tofauti za kisiasa kati ya DP na Rais zimewafanya wafuasi wao kurushiana mishale kwa kila jambo linalotokea.

Jumatatu mdahalo mwingine ulizuka kuhusu picha ya Rais iliyoomekana katiuka afisi ya DP Ruto wakati alipokuwa akifanya mkutano na Wakenya walio ughaibuni kupitia mtandao wa video.



Baada ya DP kupakia picha za mkutano huo, baadhi ya Wakenya waligundua mara moja uwepo wa picha rasmi ya Rais Uhuru Kenyatta ambayo ilikuwa karibu na ya naibu rais.

Katika hali ya kawaida, hili lisingelikuwa suala la mjadala mkubwa lakini Wakenya walitambua kwa kuona kuwa picha ya Ruto ilikuwa kubwa zaidi kuliko ya bosi wake.

Kuwekwa kwa picha hizo mbili karibu karibu kuliifanya picha ya Naibu Rais ionekane kuwa kubwa kuliko ya Uhuru, na hali hiyo ikazua mdahalo na majibizano kutoka kwa wafuasi wao.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke