Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Picha inayomuonyesha Rais Uhuru akiomba mkopo Uingereza ni feki

Ea093c2881b1cec0 Picha inayomuonyesha Rais Uhuru akiomba mkopo Uingereza ni feki

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wakati wa ziara ya siku tatu ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uingereza, aliohojiwa na mwanahabari wa Sky New, Kimberley Leonard na Sophie Ikenye wa BBC Hata hivyo, baada ya mahojiano hayo, picha ya Uhuru akiwa amesimama karibu na Kimberley, ambaye aluonea kubeba kitabu cha manjano kilichoandikwa"mkopo" ilisambaa kwenye miatndao ya kijamiiTUKO.co.ke imebaini kuwa picha hiyo ni feki na kitabu hicho kiliahiririwa na kubandikwa jina "mikopo"Picha moja ilizagaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha Rais Uhuru Kenyatta kana kwamba anaomba mkopo wakati wa mahojiano ya runinga nchini Uingereza.

Wakati wa ziara ya siku tatu ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uingereza, aliohojiwa na mwanahabari wa Sky New, Kimberley Leonard na Sophie Ikenye wa BBC.

Hata hivyo, baada ya mahojiano hayo, ya Ijumaa, Julai 30, picha ya Uhuru akiwa amesimama karibu na Kimberley, ambaye aluonea kubeba kitabu cha manjano kilichoandikwa "mkopo" ilisambaa kwenye miatndao ya kijamii.

Picha hiyo huenda ilikuwa inajaribu kudhihirisha hamu kubwa ya serikali ya Jubilee kukopa madeni.



Read also

Magazeti Ijumaa, Julai 30: Sababu za ODM Kujiondoa NASA Zatajwa

Picha feki Lakini ni kweli Rais alikuwa atafuta mkopo?

TUKO.co.ke imebaini kuwa picha hiyo ilichapishwa mara ya kwanza na balozi wa Kenya nchini Uingereza Manoah Esipisu kwenye kitandazi chake cha Twitter mnamo Ijumaa mwendo wa saa kumi na dakika 38 jioni.

Katika picha hiyo, kiongozi wa taifa alikuwa amevalia suti nyeusi akiwa amesimama kando ya Kimberley aliyevalia rinda la bluu.

Hata hivyo, kitabu cha manjano ambacho Kimberley alikuwa amekibeba mikoni mwake hakikuwa na maandishi yoyote.

Esipisu aliongezea kuwa mahojiano ya Uhuru yalikuwa yanalenga elimu, tabia nchi na chanjo za COVID-19.

TUKO.co.ke imebaini kuwa picha hiyo ni feki na kitabu hicho kiliahiririwa na kubandikwa jina "mikopo"

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke