Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pasipoti ya yapatikana miaka 30 baada ya kupotea kwenye ajali ya ndege

Pasipoti Ya Rais Salva Pasipoti ya yapatikana miaka 30 baada ya kupotea kwenye ajali ya ndege

Wed, 5 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hati ya kusafiria ya Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit imepatikana miongo mitatu baada ya mwanasiasa huyo kuhusika katika ajali ya ndege eneo la Torongo, kaunti ya Baringo.

Maafisa wa Sudan Kusini na Kenya walifanikiwa kupata eneo la ajali hiyo na pia kupata pasipoti kutoka kwa familia ya eneo hilo siku ya Jumapili, Aprili 2.

Kando na hati ya kusafiria ya Kiir, pasipoti za pamoja watu wengine waliokuwa ndani ya ndege pia zilikuwa zimehifadhiwa salama na familia hiyo ambayo ilikusanya kutoka eneo la ajali hiyo ya kushtua iliyoshohudiwa mnamo Disemba 1993.

Ndege hiyo iliyohusika kwenye ajali ilikuwa imewabeba watu sita; rubani, Rais Kiir, afisa wake wa usalama madaktari wawili wa Norway, na Muingereza.

Kulingana na ripoti, Muingereza huyo alikata roho papo hapo, huku rubani na raia wawili wa Norway wakipata majeraha mabaya ya mgongo yaliyowalemamaza na kwa sasa wanatumia viti vya magurudumu kutembea.

Waziri wa Masuala ya Rais wa Sudan Kusini, Barnaba Benjamin, akipokea hati hizo, alisema serikali inapanga kujenga hospitali katika eneo hilo kama ishara ya shukrani kwa wenyeji.

Punde baada ya ajali hiyo, wakazi walikimbia katika eneo la tukio na waliokuwa wamekwama kwenye vifusi, na kuwasafirisha hospitalini.

Rais Kiir na msaidizi wake walisafirishwa kwa lori, huku wahasiriwa wengine wakikimbizwa hospitalini kwa gari.

Arejesha mkono

Miaka 30 baada ya ajali hiyo, mnamo Jumapili, Aprili 2, Kiir aliwatuma wajumbe wake kwenye eneo la ajali ili kukutana na familia za watu ambao waliokoa maisha yao.

Ujumbe huo wa watu 15 wa Sudan Kusini uliongozwa na Waziri wa Masuala ya Rais Josephine Nopwon, Waziri wa Mazingira Thiik Kiir, mtoto wa Rais Kiir Chol Ajongo na Balozi wa Sudan Kusini nchini Kenya Chol Ajongo Balozi Bol Wek, miongoni mwa maafisa wengine.

Katika mahojiano ya awali na vyombo vya habari, familia hiyo ilisema baada ya kukusanya hati hizo walizihifadhi kwa miaka miwili bila kuzifungua ili kuona yaliyomo.

Lakini kutokana na hamu, mmoja wa wanafamilia aliamua kuangalia kulikoni na kugundua kuwa hati hizo ni za raia wa Sudan. Wenyeji hao pia walishtuka kupata pasipoti ya Kiir miongoni mwa hati hizo.

Kiir na wanadiplomasia wanne wa Sudan walikuwa wakisafiri kutoka Wilson Aiport jijini Nairobi kuelekea Kamoa, Nimule, na Sudan Kusini wakati ndege hiyo ilipoanguka kutoka futi 25,000 kutoka ardhini.

Kama njia ya kutoa shukrani, serikali ya Sudan Kusini imeahidi kujenga kituo cha kisasa cha ajali na majeraha katika Hospitali ya Misheni ya Eldama Ravine, kitakachopewa jina la Rais Salva Kiir.

Zaidi ya hayo, eneo la ajali litakuwa sehemu ya urithi wa Sudan Kusini na litabadilishwa kuwa kivutio cha watalii ambapo kutakuwa na uboreshaji wa barabara, vituo vya afya ambavyo vilitoa msaada wa matibabu, kwa kushirikiana na Kituo cha Ajali kilichopendekezwa cha Salva Kiir Mayardit huko Eldama Ravine.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live