Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Papa wakaribia kutoweka Kongo-Brazzaville

Papa Wakaribia Kutoweka Kongo Brazzaville.png Papa wakaribia kutoweka Kongo-Brazzaville

Wed, 28 Aug 2024 Chanzo: Bbc

Uvuvi usiodhibitiwa wa papa unatishia usalama wa chakula hiki katika eneo la Kongo-Brazzaville huku spishi kadhaa sasa zikiwa katika hatari ya kutoweka.

Licha ya mapishi mbadala majumbani na hata spishi za maabara, mahitaji ya papa bado yako juu barani Asia.

Nyama ya papa ni chakula kikuu na chanzo muhimu cha protini kwa watu wanaoishi katika maeneo ya pwani ya Kongo-Brazzaville.

Lakini idadi inayoongezeka ya meli katika bahari kuu na boti zisizodhibitiwa, zinapunguza idadi ya papa wa eneo hilo.

Sheria za kitaifa na kimataifa hudhibiti ni kiasi gani cha samaki kinaweza kutolewa baharini na ni wapi wanaweza kuvuliwa.

Pamoja na hayo, uvuvi usiodhibitiwa wa papa umekithiri, na kuna hatari ya kuhatarisha usalama wa chakula hiki huko Kongo-Brazzavile.

Kundi la kimataifa la meli zilizo na zisizo na bendera limekuwa likiendesha shughuli zake katika maji haya kwa miaka mingi, na hivyo kufanya iwe vigumu kutofautisha uvuvi haramu kutokana na ule wenye leseni.

"Wengi wao wanatoka Asia na nchi za Skandinavia, na pia kutoka nchi jirani za Senegal, Nigeria na Mali," anasema Oluwole Ojewale, ambaye anafanya kazi kama Mratibu wa Kikanda wa Kituo cha Kuchunguza Uhalifu uliopangwa kwa Afrika ya Kati.

Serikali ya Kongo-Brazzaville imetenga baadhi ya maeneo kwa ajili ya uhifadhi katika jaribio la kudhibiti uvuvi.

Hii imefanikiwa kuzuia baadhi ya shughuli haramu kuendelezwa eneo hilo.

Lakini ufuatiliaji wa bahari kuu kwa shughuli haramu unachukua muda mwingi na gharama ni kubwa.

Chanzo: Bbc