Wed, 1 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiongozi Mkuu wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis ameisihi dunia kuacha kupora rasilimali za Afrika jambo ambalo amesema limekuwa likisababisha migogoro mikubwa katika nchi za Afrika.
Papa ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kutua Kinshasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo alitoa hotuba iliyojaa shutuma kali za unyonyaji wa raslima za DRC kwa karne nyingi.
"Iacheni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo! Toeni mikono yenu Afrika! Acheni kuisakama Afrika, sio mgodi wa kuvuliwa au eneo la kuporwa," amesema Papa Francis.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live