Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Oscar Sudi Amtembelea Didmus Baraza, Amsihi Kurejea Siasani

77e51617636212d3 Oscar Sudi Amtembelea Didmus Baraza, Amsihi Kurejea Siasani

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Barasa alitangaza kwamba alikuwa akiondoka katika ulingo wa siasa za kitaifa kwa miezi minne ili apate kutathmini hatua atakayochukua kabla ya 2022

- Sudi alimtembelea Barasa afisini mwake kumsihi apunguze muda huo kwani ulikuwa mrefu mno

- Barasa alisema anatazamia kushikana mkono wa vigogo wengine wa siasa kutoka Mulembe kuhakikisha sauti yao ni moja wa Uchaguzi Mkuu

Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi alimtembelea mwenzake wa Kimilili Didmus Barasa kufuatia tangazo lake la kuchukua likizo fupo kutoka uwanja wa siasa.

Mnamo Jumapili, Machi 21 Barasa alitangaza kwamba alikuwa akiondoka katika ulingo wa siasa za kitaifa kwa muda ambao atatumia muda huo kutathmini hatua atakayochukua.

Kwenye ukurasa wake wa Facebook mnamo Jumanne, Machi 23, Sudi alimtembelea Barasa afisini mwake kumsihi apunguze muda aliotangaza wa miezi minne.

"Nilimtembelea rafiki yangu Didmus Barasa, mbunge wa Kimilili afisni mwake mapema leo. Nilimtemebela ili kutoa maoni yangu kuhusiana na tangazo lake la kuchukua likizo ya miezi minne kutoka siasa za kitaifa. Nimemsihi apunguze huo muda huo kwani ni mwingi mno," Sudi alisema.

Huku akisisitiza kwamba bado yeye ni mfuasi sugu wa vuguvugu la hasla linalohusiana na Naibu Rais William Ruto, mwanasiasa huyo alisema anachukua likizo ili kuunganisha eneo la Magharibi 2022 inapokaribua.

Akizungumza na waandishi wa habari mnamo Jumapili, Machi 21, Barasa alisema anatazamia kushikana mkono wa vigogo wengine wa siasa kutoka Mulembe kuhakikisha sauti yao ni moja wa Uchaguzi Mkuu.

Alisema pia atatumia mapumziko ya miezi minne kuzingatia ajenda yake ya maendeleo katika eneo bunge lake la Kimilili.

"Tunapotii mwito wa Rais Uhuru Kenyatta wa kupunguza shughuli zetu za kisiasa kudhibiti kuenea kwa COVID-19, nitatumia wakati huu kuchukua likizo kwa karibu miezi minne kusaidia taifa la Mulembe," alisema.

Barasa alibaini uamuzi wake wa kuzingatia siasa za Magharibi mwa Kenya ulitokana na jamii ya Waluhya kutofaidika na idadi kubwa licha ya kuwa moja ya makabila yenye utajiri wa kura nchini Kenya.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke