Mwanamuziki wa Marekani, Mariah Carey ameahirisha onyesho lake katika mji wa Hawaii kuhofia maambukizi ya viruso vya corona.
Katika mji huo watu watatu wamefariki dunia baada kuugua corona.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Carey amewaomba radhi mashabiki wake kwa onyesho hilo lililokuwa lifanyike Machi 10, 2020.
“Kwa masikitiko makubwa nachukua fursa hii kuwatangazia mashabiki zangu kuwa nimeamua kusogeza mbele shoo yangu hadi Novemba, 2020.”
“Nilikuwa na furaha kubwa kuja Hawaii lakini kutokana na masharti yaliyowekwa kwenye usafiri wa kimataifa kutokana na virusi vya corona, sitoweza kufanya shoo yangu tena hadi Novemba,” amsema Carey.
Wasanii wengine walioahirisha shoo zao kutokana na kuenea kwa virusi hivyo ni DJ Khalid, kundi la muziki la Korea (BTS), bendi ya US Day Green na mwimbaji Avril Lavigne.
Pia Soma
- Diamond akwepa kumzungumzia Tanasha
- Mahusiano ya Diamond, Tanasha njia panda
- Ndani ya Boksi: Siyo Mondi, Konde Boy peke yao wanaoigana
“Ilikuwa nikutanishe dunia katika ziara yangu ya kimuziki, lakini tishio la kusambaa kwa virusi vya corona limenilazimisha kuahirisha” ameandika mwimbaji huyo.
Uwepo wa virusi hivyo pia unatishia kuahirishwa tamasha la Glastonbury lililokuwa lifanyike ka siku tano mwishoni mwa Juni. Tamasha linatarajiwa kuhudhuriwa na watu 200,000 .