Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amerejea kazini baada ya kumaliza wiki moja ya kujitenga baada ya kukutwa na virusi vya Corona, ofisi yake imethibitisha hilo.
Ramaphosa, ambaye alipewa chanjo ya Johnson & Johnson mnamo Februari, alipimwa na na kukutwa na maambukizi ya COVID-19 mnamo Desemba 12 na akapokea matibabu ya dalili zisizo kali.
“Rais amerejea kazini na ataongoza kikao cha mwisho cha baraza la mawaziri kwa 2021 siku ya Jumatano,” ilisema taarifa ya ofisi ya Rais.
Katika siku chache zilizopita, milipuko ya kitaifa inayoaminika kuhusishwa na aina mpya ya kirusi cha Omicron imekuwa ikiambukiza zaidi ya watu 20,000 kwa siku, ingawa idadi ya maambukizo mapya yaliyorekodiwa ilipungua wikendi.