Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Odinga azuiwa kuingia msitu wa Shakahola

Odinga Azuiwa Kuingia Msitu Wa Shakahola Odinga azuiwa kuingia msitu wa Shakahola

Sat, 6 May 2023 Chanzo: Bbc

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amezuiwa kuingia katika Msitu wa Shakahola, Kaunti ya Kilifi, ambapo miili ya zaidi ya washiriki 100 wa dhehebu tata la kidini imepatikana.

Kiongozi wa dhehebu hilo Paul Makenzi anasemekana kuwashawishi wafuasi wake kusali na kufunga hadi kufa "ili waweze kukutana na muundaji wao".

Bw, Raila alifika eneo hilo akiandamana na viongozi kadhaa wa Pwani wa Munngano wa upinzani wa Azimio la Umoja, One Kenya.

Waziri Mkuu huyo wa zamani na washirika wake walipokelewa na maafisa wa polisi waliokuwa wakisimamia eneo la tukio na kutembezwa kwa muda mfupi na kupewa maelezo machache kuhusiana operesheni hiyo.

''Niliambiwa kwamba siwezi kufika huku na kwamba naweza tu kutembezwa na kuongozwa na wanachama wa kamati ya usalama ya Bunge. Hiyo ni aibu. Sihitaji kuandamana na wabunge, Nalaani kilichotokea hapa leo.'' alisema.

Huku hayo yakijiri kamanda wa operesheni ya kuchunguza vifo hivyo, Bw Peter Ndung’u, alimtaka Raila kutafuta kibali kutoka kwa Inspekta Jenerali iwapo angetaka kuingia msituni, kulingana na taarifa za vyombo vya habari vya ndani.

"Nataka kufikia msitu ili niweze kuona makaburi, siwezi kusafiri mwendo mrefu hivi na kurudi bila kufika eneo la tukio," Raila alisema.

Chanzo: Bbc