Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

ODM yatangaza rasmi kuondoka NASA

Bf3e1c384e1e1871 ODM yatangaza rasmi kuondoka NASA

Fri, 30 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Chama cha Chungwa kilitangaza kuwa kitamuandikia barua Msajili wa Vyama vya Siasa kuwasilisha uamnzui wake wa kuondoka katika muungano wa NASAKatibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna alitangaza hayo baada ya mkutano wa NEC ulioongozwa na RailaTangazo hilo linajiri siku moja baada ya kinara wa ODM Raila Odinga kushinkizwa kugawa pesa za vyama hivyo na vigogo wenazake wa NASAKatibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna Alhamisi, Julai 29, alitangaza kwamba chama hicho kilifanya uamuzi wa kuondoka rasmi katika muungano wa National Super Alliance (NASA).

Chama hicho cha chungwa ni cha pili kuutema muungano huo baada ya kile cha Wiper kuchukua hatua hiyo.

Katika taarifa, Sifuna alifichua kwamba chama hicho kilifanya mkutano Alhamisi, Julai 29 na kuamua kutafuta marafiki wapya.

"Tunakusudia kuanza mpango wa kujenga ushirikiano mpya na kupanua mazungumzo yanayoendelea na wenzetu hadi kule mashinani," taarifa hiyo ilisema.

Wakati uo huo, Sifuna alitupilia mbali ripoti kwamba ODM iliwahonga washirika wengine wa kisiasa kwa nia ya kuwashawishi wasalie katika mungano huo.



Read also

Magazeti Jumatano, Julai 28: Mt Kenya Waahidi Kulipa Deni la Raila 2022

"Chama chetu kimesikitishwa na taarifa zinazosambazwa na baadhi ya washirika wetu wa zamani kwamba tumewalipa baadhi ya washirika wengine hela ili kuwashawishi wasalie katikamuungano, huo ni uongo mtupu."

Sifuna aliongeza kuwa chama hicho kilifanya maamuzi hayo ili kujijenga katika siku za usoni na kuunda marafiki wengine waliuo na wazo sawia na la chana cha ODM.

Iwapo vyma vitatu vilivyoafikiana kuunda muungano huo vitaondoka basi ina maana kwamba NASA itakuwa imezikwa katika kaburi la sahau na mikataba hiyo kuvunjwa.

Muungano wa NASA umekabiliwa na changamoto tangu 2018 kutokana na kutokuaminiana kati ya vyama Wiper Democratic Movement, ODM, ANC na Ford Kenya.

Tangazo hilo linajiri siku moja baada ya kinara wa ODM Raila Odinga kushinkizwa kugawa pesa za vyama hivyo na vigogo wenazake wa NASA.

Je, unayo taarifa ya kusisimua mbayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Kivutha Kibwana Amsuta Kalonzo Baada ya Kumtema Chamani 2022 Inapokaribia
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke