Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

ODM yalambisha Jubilee sakafu kwenye uchaguzi mdogo wa Bonchari

5f28d33b5075f8b2 ODM yalambisha Jubilee sakafu kwenye uchaguzi mdogo wa Bonchari

Wed, 19 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Oimeke aliibuka mshindi baada ya kupata kura 8,049 katika uchaguzi huo ulioandaliwa Jumanne, Mei 18

- Mgombea wa Chama cha Jubilee, Zebedeo Opore alikuwa wa pili na kura 7,279 akifuatwa na mgombea wa UDA, Teresa Bitutu ambaye alipata kura 6,964

- Ushindi wa Omieke ulizingirwa na fujo wakati wa uchaguzi huo huku akiwakashifu polisi kwa kuwahangaisha wafuasi wake

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), imemtangaza mgombea wa ODM Pavel Oimeke katika uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Bonchari kama mshindi.

Oimeke, ambaye ni mkurugenzi mkuu wa zamani wa Tume ya Kudhibiti Kawi (EPRA) aliibuka mshindi baada ya kupata kura 8,049 katika uchaguzi huo ulioandaliwa Jumanne, Mei 18.

Mgombea wa Chama cha Jubilee, Zebedeo Opore alikuwa wa pili na kura 7,279 akifuatwa na mgombea wa UDA, Teresa Bitutu ambaye alipata kura 6,964.

Ushindi wa Omieke ulizingirwa na fujo wakati wa uchaguzi huo huku akiwakashifu polisi kwa kuwahangaisha wafuasi wake kufuatia kukamatwa kwa mmoja wa maajenti wake katika kituo cha kupiga kura cha Nyamare.

Visa vya wizi wa kura pia viliripotiwa pamoja na wapiga kura kuhongwa ambavyo vilithibitishwa na Kamanda wa Polisi eneo la Nyanza Karanja Muiruri ambaye alisema baadhi ya washukiwa walikamatwa.

Kuhusu kunyanyaswa kwa wapiga kura, Karanja alisema ulinzi huo mkali haukuwa na ubaguzi.

“Tulitumwa kutekeleza amani na hatuna chuki na yeyote,sisi hatubagui Mkenya yeyote” Karanja alinukiliwa na KBC.

Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga pia kupitia Twitter pia aliwakasifu polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi katika chaguzi ndogo za Bonchari na Juja akitaja kama utumizi mbaya wa mamlaka kutoka kwa baadhi ya maafisa wakuu serikalini.

Omieke sasa ameibuka mbnge wa kwanza kuchaguliwa kupitia tikiti ya ODM tangu 2018 katia kaunti ya Kisii ambayo ni ngome ya chama hicho.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke