Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyumba ya Mwandishi wa Habari Homa Bay Yateketea Moto Usiku

50934a39fbc3d0a1 W Nyumba ya Mwandishi wa Habari Homa Bay Yateketea Moto Usiku

Fri, 26 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mali ya thamani isiyojulikana imeharibiwa mjini Homa Bay katika kisa cha moto

- Moto huo uligeuza nyumba ya Florence Ochieng kuwa majivu

- Florence Ochieng alisema kuwa moto uliharibu mali yake yenye thamani ya zaidi ya KSh 600k

Mali yenye thamani isiyojulikana iliharibiwa katika tukio la moto ambalo liliteketeza nyumba ya makazi ndani ya mali katika Homa Bay Town.

Tukio hilo, ambalo lilifanyika Jumatano, Machi 24, lilipelekea nyumba ya Florence Ochieng, mwandishi wa habari wa Homa Bay na majirani zake wawili kusalia majivu.

Akizungumza na TUKO.co.ke Florence Ochieng alisema kuwa moto uliharibu mali yake yenye thamani ya zaidi ya KSh 600k.

Alisema kuwa kila kitu kiliteketea kutokana na moto ikiwemo mabegi yaliyokuwa yamehifadhi stakabadhi zake na za watoto wake wanne.

Mwanahabari huyo alisema kwamba wakati moto huo ulipozuka hakuwepo nyumbani ila mfanyakazi wa nyumbani na wanawe walikuwepo bomani humo.

"Sikuwa nyumbani wakati tukio hilo lilipoanza, niliarifiwa na majirani na nikakimbia kuona kilichokuwa kinaendelea, nyumba yangu ilikuwa tayari imeungua, hakuna kilichookolewa," Ochieng alisema.

Mwanhabari huyo wa Redio Lake Victoria alisema mtoto wake wa mwaka mmoja, ambaye alikuwa amelala wakati wa mkasa huo alilemewa na moshi ambapo alikimbizwa hospitalini na kitibiwa.

Ochieng alidokeza kwamba alilazimika kulala usiku nyumbani kwa rafiki yake.

Alikariri kwamba tukio hilo lilikuwa limemwacha hohehahe asijue pa kuanzia.

"Nimeachwa hivi bila kitu na watoto wangu wadogo, na sijui nifanye nini na nani nimuombe msaada. Nimekwama," alisema.

Naibu Chifu wa Asego Tom Ondiek alisema kuwa chanzo cha moto huo hakikujilikana ila alishuku huenda ikawa hitilafu ya nguvu za umeme.

Ondiek alisema moto huo ulikabiliwa baada ya wenyeji kukabiliana nao wakisaidiana na wazima moto kutoka kituo cha Homa Bay na wazima.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke