Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyeri: Mwanafunzi wa kidato cha 4 afariki dunia baada ya kuzirai

0fgjhs4erjaaard4k Nyeri: Mwanafunzi wa kidato cha 4 afariki dunia baada ya kuzirai

Fri, 30 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwanafunzi wa kidato cha nne amefariki dunia baada ya kuzirai akiwa njiani akielekea shuleniMwalimu mkuu wa shule ya upili ya Othayo E. M Waititu alisema amewasiliana na familia yake na mipango ya mazishi tayari imeshaanzaUchunguzi kufuatia kifo cha mwanafunzi huo umeanzisha piaMwili wake umehifadhiwa katika makafani ya kituo cha afya cha Consolata Nursing HomeMwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya upili ya Othaya kaunti ya Nyeri ameripotiwa kuzirai na kisha kufariki dunia alipokuwa akisafiri kwenda shuleni.

Hata hivyo, haijabainika ni nini kilisababisha kifo chake lakini maafisa wa polisi wameanzisha uchunguzi.

Akithibitisha kifo chake, mwalimu mkuu wa shule hiyo E. M Waititu alisema amewasiliana na familia yake na mipango ya mazishi tayari imeshaanza.

" Alikuwa mmoja wa wanafunzi bora zaidi masomoni, tunasikitika kwamba kifo chake kimetokea ghafla, marehemu alizira na kisha akafariki dunia kwa njia tatanishi," Waititu aliambia waandishi wa habari.



Read also

Mumewe Caroline Kangogo Aomba Kutowahutubia Waombolezaji

Marehemu alitambulika kwa majina Katali Mutinda kulingana na taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Facebook wa shule hiyo.

" Tunaomboleza kufuatia kifo cha mwanafunzi wetu mmoja, tungependa muomboleze nasi, matayarisho ya mazishi inaendelea na pia uchunguzi wa maiti unapaswa kufanywa," Taarifa kutoka kwa shule hiyo ilisoma.

Kimathi alifariki dunia pindi alipofikishwa katika hospitali ya Kenyatta National Hospital- Othaya Annex .

Mwili wake umehifadhiwa katika makafani ya kituo cha afya cha Consolata Nursing Home.

Kimathi alikuwa akifadhiliwa na Benki ya Equity baada ya kufanya vema katika mtihani wa kitaifa wa darasa la nane, KCPE.

Familia yake imesema kifo chake ni pigo kubwa kwa wazazi ikizingatiwa kwamba haijiwezi na ilikuwa na matumaini kwamba angeisaidia akifaulu maishani siku moja.

Kulingana na taarifa tulizopokea hapa TUKO.co.ke, mamake amekuwa mgonjwa kwa miaka mitatu na madaktari wameshindwa kubaini aina ya ugonjwa anaougua.



Read also

Nyeri: Mwanafunzi wa Kidato cha Nne Azirai na Kuaga Dunia Akielekea Shuleni

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke