Uzinduzi wa filamu ya ‘No Time to Die’ umesogezwa mbele hadi Novemba kutokana na kuwapo kwa tishio la kusambaa kwa virusi vya corona.
James Bond alitoa ufafanuzi huo kwa mashabiki wake kupitia barua ya wazi aliyoiweka katika kurasa zake mitandaoni, akiwajibu mashabiki waliouliza kama kweli filamu hiyo itatoka Aprili tatu kama walivyoahidi.
Katika taarifa hiyo Bond alisema kuwa wamesimamisha kila kitu hadi Novemba, kutokana na kuwapo kwa virusi vya corona ambavyo vinasambaa duniani.
Trela ya filamu hiyo ilikuwa itoke Aprili tatu, lakini kwa mujibu wa taarifa ya Bond haitatolewa kutokana na kuwapo kwa taharuki ya ugonjwa huo.