Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nitatumia mbinu nyingine kupitisha BBI, Raila adai

D5391d94c13837ca Nitatumia mbinu nyingine kupitisha BBI, Raila adai

Wed, 21 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila amedokezea kutafuta njia mbadala iwapo mahakama ya rufaa itafutilia mbali BBIRaila alisema kiu cha Wakenya kutaka mabadiliko ya uongozi hakiwezi kukatizwa na hivyo atatumia mbinu tofauti kupitisha BBIKauli ya Raila inakujia wakati Wakenya wakiendelea kusubiri kwa hamu na ghamu uamuzi wa mahakama ya rufaa kuhusu hatma ya BBI

Kiongozi wa Orange Democratic Movement (ODM), Raila Odinga amedokezea kutafuta njia mbadala iwapo Mswada wa Kurekebisha Katiba 2022 kupitia Mpango wa Maridhiano(BBI) utasitishwa na mahakama.

Akizungumza katike eneo la Dabaso, Kilifi Kaskazini, Jumanne, Julai 20, Raila alisema kiu cha Wakenya kutaka mabadiliko ya uongozi hakiwezi kukatizwa akidokezea kutumia mbinu tofauti ambayo hakufafanua kupitisha BBI.

"BBI ambayo tulileta ilikuwa ya kubadilisha namna Kenya inaongozwa na kuleta usawa kuhusiana na maendeleo na kaunti kutengewa pesa zaidi. Hii ndio maana tunataka BBI iendelee. Hata kama inapigwa vita tutatafuta mbinu ili iweze kupita," alisema Raila kama alivyonukuliwa na gazeti la The Standard.



Read also

Mungu Alimponya Raila Kutokana na Corona kwa Sababu Ana Mipango Mizuri Naye, Junet Mohamed

Rufaa ya BBIKauli ya Raila inakujia wakati Wakenya wakiendelea kusubiri kwa hamu na ghamu uamuzi wa mahakama ya rufaa kuhusu hatma ya BBI.

Hii ni baada ya wakereketwa kukataa rufaa dhidi ya uamuzi wa Makama Kuu iliyoharamisha mswada huo kufuatia kesi ya wanaharakati na mashirika kuupinga.

Mahakama ya Rufaa sasa inatarajiwa kutoa uamuzi wake Agosti 20, baada ya kumaliza kusikiliza rufaa zilizowasilishwa na Rais Uhuru Kenyatta, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na kiongozi wa ODM, Raila Odinga.

Raila asisitiza BBI itabadilisha uongozi KenyaAkizungumza katika kaunti ya kwale mnamo Jumapili, Julai 18, Raila alilaumu wanaopinga BBI akisema wanapotosha Wakenya kwamba gharama ya kuongeza serikali itaongezeka wakiupitisha.

Kinara huyo wa Upinzani alitetea mswada huo akisema utapunguza gharama ya kuendesha serikali kwa sababu mawaziri wengi watakuwa wabunge ambao hawatalipwa mishahara zaidi.

Raila alisema wadhifa wa waziri mkuu utashikiliwa na mbunge na kwa hivyo serikali haitamlipa mshahara zaidi ya mbunge.



Read also

Mbunge Junet Mohamed Amshauri Rais Uhuru Amfukuze DP Ruto

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke